Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.

Awali ya yote naomba nipongeze kiteno cha Serikali kuwarjesha watumishi. Napongeza sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya hilo kwa maana ya ukurasa wa saba unaozungumzia mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Tano kuna eneo linalozungumzia kujenga ari ya uzalendo kwa kuilinda na kuisemea nchi yetu bila woga, kudumisha amani, utulivu na mshikamano. Eneo hili bahati nzuri jana tulibahatika kupata semina ya Kamati inayoshughulikia masuala ya mauaji ya Kimbari kwa maana ya genocide. Tumeambiwa sisi kama Wabunge, tunayo nafasi kubwa ya kudumisha amani, lakini ni vitendo vidogo vidogo ambavyo vikiachiwa, vitendo hivyo vikiendelea bila ustaarabu vinazaa mauaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini hiyo, kama haitoshi tunaambiwa tushughulikie mapema kwa maana ya conflict early warning system. Tukishughulikia mapema tutaendelea kutengeneza nchi yenye amani na utulivu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukurasa wa 54 na 56 unazungumzia suala la afya. Katika eneo hili la afya naomba nijikite kwa maana ya Hospitali ya Mkoa ya Katavi. Bajeti iliyotengwa takribani shilingi bilioni 11, kwa suala zima la utoaji wa fedha na nilikuwa naomba Waziri Mkuu anisaidie katika hili, leo asubuhi nilisikia taarifa nchi ikipongezwa kwa maana idadi ya wagonjwa wanaopelekwa nje ya nchi wanaanza kupungua, ni jambo jema.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini tukiipongeza nchi kwa hilo, kule Katavi unapoongelea ujenzi wa hospitali ya mkoa ambayo tunahitaji takribani shilingi bilioni 11 kwa kasi ya utoaji fedha, mara mmepewa shilingi milioni 500, mmebahatisha shilingi bilioni moja, maana yake tunakwenda miaka 11 ili kumaliza ujenzi wa hospitali hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa naomba sana. Na ninaliomba hilo kwa sababu, unafahamu Jiografia, umbali kule tuliko na bila msaada wa hilo na kwa wakati huu hospitali ya Manispaa ya Mpanda ndio inabeba dhamana ya kuwa hospitali ya mkoa, imeleemewa sana, inahudumia takribani Wilaya tatu, Majimbo matano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nilikuwa naomba sana hata pale tunapozungumzia kuwezesha fedha, ili kupunguza mzigo nilikuwa naomba hilo tujaribu kuliangalia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini naomba kwa maana ya hotuba ya Waziri Mkuu ukurasa wa 31 mpaka 32 unazungumzia masuala ya umwagiliaji kwa ujumla wake kwa kupitia kilimo. Tunao mradi mkubwa wa Mwamkuro, mradi huu kwa maana ya bajeti ya mwaka 2013/2014 ulitengewa milioni 294 na fedha hizo zilikuwa zimelenga kukamilisha kilometa mbili, lakini umbali wa mradi mzima ni kilometa tatu. Eneo hilo ni ukanda mzuri ambao una uzalishaji mkubwa wa kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilichokuwa nakiomba, ili thamani ya fedha iweze kuonekana kwa kiwango kile cha fedha kilichotengwa ambacho kimekwenda kukidhi kilometa mbili tu hatutaweza kuiona thamani ya fedha. Ni vizuri fedha ikatengwa ya kutosha ambayo itufikishe kwenye zile kilometa tatu zilizokusidiwa na ninalisema hilo makusudi kwa sababu kwa kupitia kilimo cha umwagiliaji na eneo lile ni zuri lina rutuba ya kutosha tutaweza kuzalisha mazao ya kutosha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nitoke hapo, kwenye suala zima la nishati. Nafahamu jitihada za Serikali na kwa maana ya Mkoa wa Katavi tunazo mashine mbili pale zinasaidia japo umeme unakatikakatika, lakini muarobaini wa kutatua matatizo ya umemeā€¦

(Hapa Kengele ililia kuashiria kuisha muda wa Mzungumzaji)