Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Augustine Vuma Holle

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. AUGUSTINE V. HOLLE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru, ahsante kwanza awali ya yote nipende kupongeza na niseme naunga mkono hoja ya hotuba ya Waziri Mkuu.

Pia napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kutupa uhai huu, Waziri Mkuu hotuba yako ni nzuri sana. Imeeleza ni namna gani ambavyo Serikali imejipanga na kujipambanua lakini namna gani ambavyo imekuwa ikitekeleza Ilani yetu ya Chama cha Mapinduzi. Hongera sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nijikite kwanza na yale mambo ambayo yapo kwenye Jimbo langu. Nipende kushukuru Serikali, nipende kumshukuru Mheshimiwa Rais kwa hela ambazo ametupa jimbo la Kasulu Vijijini shilingi milioni 500 kwa ajili ya ukarabati wa kituo cha afya pale Nyakitonto lakini pia shilingi milioni 200 kwa ajili ya ukarabati wa kituo cha afya pale Hospitali ya Muyowozi lakini nipende kushukuru Serikali pia kupitia Waziri wa Afya kwa namna ambavyo ananipa ushirikiano pamoja na TAMISEMI kwenda kuanzia Hospitali ya Wilaya pale Muzye, pale mkandarasi atamaliza kazi yake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye suala la viwanda nipende kumwomba Mheshimiwa Mwijage na Serikali kwa ujumla kwamba kuna mwekezaji alikuja kwetu pale Kigoma Sugar kwenye Jimbo langu. Mwekezaji yule alipewa ardhi ili aweze kufanya kilimo cha miwa na kuanzisha kiwanda, lakini ameshindwa kufanya hivyo na ameenda kinyume na mkataba. Sasa tunaomba Serikali iweze kumnyang’a mtu huyu eneo lile na hatimaye waweze kuwavutia uwekezaji kwa watu wengine ili kwamba watu wengine waweze kujitokeza na kufanya kilimo cha miwa na hatimaye kiwanda cha sukari tuweze kuwanufaisha watu wa Kasulu Vijijini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye Maliasili na Utalii, tarehe 20 Julai kama sikosei Mheshimiwa Rais alikuja Wilaya ya Kasulu, pomaja na mambo mengine ambayo alisema aliruhusu wananchi waendelee kulima sehemu ya kipande cha msitu wa Makere kusini yaani Kagerankanda na alifanya hivyo kutokana na mateso makubwa ambayo wananchi walikuwa wakiyapata kwa kupigwa na watu wa Maliasili na Utalii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, cha ajabu wako watu ambao sijajua kiburi wanakitoa wapi, wanaendelea kuwanyanyasa watu ambao wanaenda kulima Kagerankanda, hii haikubaliki ni kinyume cha maelekezo ya Mheshimiwa Rais. Kwa hiyo, niombe chonde chonde Mheshimiwa Kigwangalla umenipa ushirikiano katika hili, tulimalize hili wananchi waendelee kulima vizuri na hatimaye waweza kufaidi kauli ya Mheshimiwa Rais.

Mheshimiwa Waziri Mkuu chapa kazi, yasema nguvu ya mamba iko kwenye maji; na maji yako wewe ni sisi tupo, tuko nyuma yako tunaona kazi kubwa ambayo wewe pamoja na Mheshimiwa Rais mnaifanya kwa ajili ya Watanzania leo haya mambo mengine makelele hayo tuachane nayo nawaambia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimekuwepo Bungeni hapa kwa muda wa miaka kama miwili na kidogo. Moja ya kitu ambacho nimegundua humu Bungeni ni kwamba tunayo macho mawili ya kibinadamu. Liko jicho ambalo ni zima lenye afya lakini liko jicho ambalo lina chongo humu ndani. Nasema hivyo kwa sababu gani, haiwezekani watu tunawambia Serikali inajenga na imeanza ujenzi wa Standard Gauge Railway kutoka Dar es Salaam na Mkandarasi amepatikana na ujenzi umeanza lakini watu wanabeza wanaona kama ni reli ya udongo.

Mheshimiwa Mwenyekiti,haiwezekani tuwaambie watu kwamba tunanunua ndege na ndege zimekwishafika tatu zimeonekana, lakini watu wanazibeza wanaona kama ni parachute sio ndege. Tunawaambia watu kwamba hawa watu huyu kwamba hao viongozi wenu wana matatizo, wanafanya makosa wanaenda kinyume na utaratibu na wanapaswa washughulikiwe kama wahalifu wengine wao wanaona hapana wanaonewa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa nipende kusema kitu kimoja, ifike pahala tujitahidi sana kutenganisha kati ya kazi ya vyombo na Mheshimiwa Rais maana mtu anafanya makosa, anaenda kinyume na utaratibu, anavunja sheria halafu akianza kushughulikiwa, unakuta watu wanasema kwamba anashughulikiwa na Mheshimiwa Rais nani kasema? Nani kasema, hii ni nchi ambayo inaongozwa kwa mujibu wa sheria mtu yeyote anapokuwa amefanya makosa inapaswa ashughulikiwe kama mhalifu mwingine. Haya maneno ya watu kukimbia kwenda wapi kwenda kwa mabwana zao kutafuta sijui…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha muda wa Mzungumzaji)