Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. LUCIA U. M. MLOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niachangie hoja hii kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, elimu. Kumekuwa na ongezeko kubwa la usajili wa watoto wengi wa darasa la kwanza, lakini hakuna ongezeko la Walimu, madarasa na madawati. Naomba kuishauri Serikali kuajiri Walimu wa kufundisha, hasa madarasa ya awali, darasa la kwanza na la pili, ambapo Walimu wanaofundisha madarasa hayo ni wachache na shule nyingine hakuna kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia, naishauri Serikali kuwapa moyo wananchi ambao wamejitolea kujenga madarasa, lakini wanakatishwa tamaa na viongozi wanaposhindwa kuwasaidia wanapokuwa wamejenga majengo hayo hadi kufikia kiwango fulani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na kusimamishwa wazazi kuchangia, kumejitokeza tatizo kubwa la kupunguza mitihani ya mwaka mfano, katika Mkoa wa Njombe kila mwaka ratiba ya mitihani ya mock hutolewa mapema mwanzoni mwa mwaka, lakini safari hii haikutolewa ratiba hiyo. Hadi mwezi huu Aprili hakuna taarifa yoyote ya mitihani ya mock. Naomba suala hili lifuatiliwe ili watoto wetu waweze kujipima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la maji ni kubwa sana nchi nzima. Kuna maeneo ya vyanzo vizuri vya maji na mito ya kutosha, lakini bado maeneo hayo yana matatizo makubwa ya maji. Mfano, Mkoa wa Njombe kuna vyanzo vya maji vya kutosha, pia mito ya kutosha, lakini bado kuna tatizo kubwa la maji, hasa maeneo ya Makambako, Wanging’ombe, Njombe Mjini. Naishauri Serikali kuwa na mawasiliano ya karibu na wananchi wa maeneo husika ili waweze kuweka mikakati ya kuibua njia za kupeleka maji katika maeneo yao. Pia, wawawezeshe kwa kuwapelekea wataalam na vifaa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi hiyo ya maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia, kuna tatizo kubwa la uchakavu wa mabomba ambayo yanapasuka kila siku. Mfano, hapa Dodoma maeneo ya Kisasa, mabomba yanapasuka kila siku na kusababisha upotevu wa maji. Naomba mabomba hayo yabadilishwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ulinzi na usalama; kumekuwa na matukio yanayohatarisha maisha ya raia. Kwanza kumekuwa na mauaji maeneo mengi ya nchi yetu, watu wamekuwa wakiuawa na kuwekwa kwenye mifuko na kutupwa baharini. Naiomba Serikali ichukue hatua haraka ya kukomesha mauaji hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.