Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Pascal Yohana Haonga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbozi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hotuba ya Waziri Mkuu ukurasa wa 10 limezungumzwa suala la chaguzi ndogo za Wabunge zilizofanyika katika majimbo matano na Madiwani katika kata 59. Chaguzi hizi zilitawaliwa na vurugu, dhuluma, pamoja na ukiukwaji wa haki za binadamu. Viongozi na wanachama wa chama cha CHADEMA walikamatwa na kubambikiwa kesi, wengine waliumizwa kwa kukatwa mapanga na wengine kupoteza maisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano Katibu wa CHADEMA, Kata ya Hananasifu Kinondoni aitwaye Daniel aliuawa wakati wa uchaguzi mdogo wa Jimbo la Kinondoni. Hadi sasa hakuna taarifa zozote za kukamatwa kwa wauaji. Kitendo hiki kinalifanya Taifa letu kuwa siyo sehemu salama tena kama zamani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mauaji ya mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Usafirishaji, Akwilina Akwilin. Pia, nchi yetu imeonesha kwamba, siyo sehemu salama tena. Mambo haya yasipodhibitiwa yanajenga chuki na visasi katika Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia, Serikali iliahidi milioni 50 kila kijiji, suala ambalo halijatekelezwa hadi sasa. Huu ni mwaka wa tatu tangu Serikali itoe ahadi, lakini jambo hili halizungumzwi tena. Siyo jambo jema Serikali kuahidi halafu ikashindwa kutekeleza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, miradi mingi ya maji nchini imesimama kwa sababu ya kutopeleka fedha. Mfano Mji Mdogo wa Mlowo uliopo Jimbo la Mbozi, kuna mradi wa maji wa milioni 400 na certificates zilishatumwa Wizarani, lakini fedha hazijatolewa na kusababisha mradi kusimama
kwa muda mrefu sasa. Naikumbusha Serikali kupeleka fedha za mradi huu ili ukamilike na wananchi wapate huduma ya maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.