Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Mwantum Dau Haji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la Muungano wetu na changamoto. Kwanza ni suala la biashara na ajira katika Taasisi za Muungano, napenda kuishauri Serikali kuhusu masuala haya bandari tuachiwe biashara ndogondogo tupitishe bila pingamizi. Pili, ajira nazo zikitokea kuhusu Muungano tupewe japo kama Tanzania watu kumi basi tupatiwe watu wanne kwa Zanzibar.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Serikali kuhamia Dodoma. Utekelezaji wa zoezi hilo unaimarika Watumishi wa Umma na Taasisi mbalimbali wamehamia Dodoma.

Miundombinu hasa barabara za ndani hasa kama Area D’ barabara ni mbovu mno. Naishauri Serikali yangu izione barabara hizo au TBA nao wanahusika kuhusu hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la uwezeshaji wananchi kiuchumi. Naishukuru Serikali kuanzisha Mfuko wa Uwezeshaji ambao unatoa mikopo kupitia vikundi vya vijana, wanawake, wazee, watu wenye ulemavu na makundi mengine. Naomba Mfuko huu uimarike uzidi kusaidia mpango huu hasa kusaidia wanawake ili wajikwamue kiuchumi na kuondoa umaskini na kudhalilika kijinsia pia vijana kupata asilimia 10.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la vita dhidi ya dawa za kulevya. Madawa ya kulevya nchini ni tatizo. Vijana tunaowategemea ndiyo wanaoathirika hapa nchini licha ya Serikali kujitahidi juu ya suala hili bado ijitahidi kupatiwa vituo vya Sober House ili kuwapatia masomo na ujasiriamali waondokane na kadhia hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu barabara za vijijini na mjini. Wakala wa Barabara TARURA, ufanisi wao ni mdogo hawajengi barabara za kiwango wanakuwa wanafyeka tu, madaraja mabovu yakipata dhoruba za mvua yanakatika. Serikali sasa inaanza kupata hasara kubwa. Nashauri Serikali yangu Halmashauri ziwasimamie TARURA utendaji wao wa ujenzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru hotuba hii ya Mheshimiwa Waziri Mkuu iliyojaa mashiko na mambo yote nasema ahsante na naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.