Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Catherine Nyakao Ruge

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. CATHERINE N. RUGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia hotuba hii ya Waziri Mkuu. Nianze na suala la utawala bora.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi yoyote duniani ili iwe na maendeleo, lazima ifuate sheria na taratibu ilizojiwekea kama nchi. Hivi karibuni tumeona sheria zetu zikivunjwa. Mfano, Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya wamekuwa na mamlaka makubwa na bila kufuata sheria wamekuwa wakitoa amri kwa viongozi mbalimbali wakiwemo Wabunge kuwekwa ndani kinyume cha sheria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia pia, kuhusu nishati ya gesi. Miaka mitatu iliyopita wananchi waliaminishwa kuwa ujenzi wa bomba la gesi kutoka Mtwara kuja Dar es Salaam utaenda kutatua tatizo la nishati kabisa nchini, lakini katika hotuba ya Waziri Mkuu jambo hili halijazungumziwa kabisa; na kinachoendelea sasa hivi ni mradi wa Stieglers’ Gorge. Je, ni kwa nini Serikali imeamua kubadilisha kipaumbele chake toka kwenye umeme wa gesi kwenda kwenye umeme wa maji, huku tukifahamu Serikali imeshatumia pesa nyingi za walipakodi kuwekeza kwenye mradi wa gesi asilia?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mradi huo bado haujawa fully utilised, kwani mpaka sasa ni 6% tu ya bomba la gesi linatumika. Naitaka Serikali iwaambie Watanzania, ni kwa nini imehamisha focus toka kwenye umeme wa gesi asilia kwenda kwenye umeme wa maji?

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda pia, kuchangia kuhusu hali ya uchumi iliyozungumziwa ukurasa wa nane katika hotuba ya Waziri Mkuu. Hotuba inaonesha uchumi wa nchi yetu unakua kwa asilimia 6.8 kwa kiwango cha juu kuliko nchi zote za Ukanda wa Afrika Mashariki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sina shaka na takwimu hizo, ila tatizo langu lipo kwenye jinsi gani hali ya uchumi iko reflected kwa wananchi wa kawaida. Wananchi wana hali mbaya sana hata kupata milo mitatu ni tatizo. Je, huo uchumi unaokua unawanufaisha vipi wananchi, kama wananchi hawawezi hata kula milo mitatu kwa siku?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.