Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Kiteto Zawadi Koshuma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. KITETO Z. KOSHUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hotuba hii, ukurasa wa 23, imeonesha kuwa tayari Mheshimiwa Rais amekwishasaini Sheria ya Kuunganisha Mifuko ya Hifadhi ya Jamii ambayo ilitungwa na Bunge. Kufuatia kusainiwa kwa sheria hiyo inatakiwa ianze kutumika ili kuhakikisha wadau wa mifuko hiyo wanapata stahiki zao hasa pale wanapoacha kazi kwa kustaafu au kwa kuachishwa kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, concern kubwa ya wadau ni formula ya kikokotoo kitakachotumika kwa ajili ya kulipa mafao ya kustaafu au kuacha kazi kwani katika sheria kikokotoo hakikuwekwa na Serikali ilisema kuwa formula itawekwa katika kanuni. Uzoefu unaonesha kuwa sheria nyingi zinazopitishwa na Bunge na kusainiwa na Mheshimiwa Rais zinachelewa kutungiwa kanuni. Hivyo basi, Serikali ijitahidi kutunga kanuni mapema ili sheria iweze kuwa effected.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Serikali itoe elimu kwa wadau wa mifuko hii ili ku-raise awareness kuhusu mabadiliko ya sheria hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.