Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Dr. Advocate Damas Daniel Ndumbaro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songea Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. DKT. DAMAS D. NDUMBARO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya Awamu ya Tano imefanikiwa na inastahili pongezi kwa kufanya mambo yafuatayo katika Jimbo la Songea Mjini. Ujenzi wa barabara kilomita kumi kwa kiwango cha lami, kuboresha elimu na kuboresha huduma za afya. Pamoja na hayo Jimbo la Songea Mjini linakabiliwa na changamoto zifuatazo:-

(i) Ukosefu wa vituo vya afya katika Kata za Ruvuma, Lilambo na Ndilimalitembo;

(ii) Ukosefu wa ambulance na X-ray katika Kituo cha Afya cha Mjimwema ambacho kinahudumia zaidi ya wagonjwa 100,000 kwa mwaka;

(iii) Ujenzi wa Mtwara Corridor by-pass katika eneo la Jimbo la Songea Mjini;

(iv) Upatikanaji usioridhisha wa pembejeo za kilimo kama vile mbolea na bei elekezi ambayo inabadilika kila kukicha;

(v) Soko lisilo na uhakika la mazao kama vile mahindi na mbaazi;

(vi) Ukosefu wa barabara ya uhakika (lami) inayounganisha Mji wa Songea na Jimbo la Lichinga – Msumbiji;

(vii) Ukosefu wa barabara ya lami inayounganisha Mkoa wa Ruvuma na Morogoro;

(viii) Ukosefu wa viwanda vya kusindika bidhaa za kilimo; na

(ix) Malipo ya fidia kwa wananchi waliohamishwa Songea Airport; wananchi wa eneo la EPZA Mwenge mshindo na wananchi wa eneo la Bonde la Mto Luhira.