Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora

Hon. Kabwe Zuberi Ruyagwa Zitto

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Kigoma Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora

MHE. KABWE Z. R. ZITTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia hotuba zenye mafungu mbalimbali ya Wizara ya TAMISEMI, mafungu matatu na Wizara ya Ofisi ya Rais, Utawala Bora pamoja na Utumishi, na nitachangia maeneo kama matatu/manne tu kutokana na muda jinsi itakavyokuwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kwanza ambalo nataka kulichangia ni la upande wa Fungu 30, Ofisi ya Rais Cabinet Secretariat ambapo ni pamoja na Fungu 20 ambapo ndipo Idara ya Usalama wa Taifa ipo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka jana tarehe 21 Julai, Rais alifanya ziara Mkoani kwetu Kigoma, siku moja kabla ya Rais kufika katika Wilaya ya Kibondo, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Ndugu Simon Kanguye aliitwa Ofisini kwa Mkurugenzi akakutana na District Security Officer (DSO) wa Kibondo na toka siku hiyo Mwenyekiti huyu wa Halmashauri na Diwani hajulikani alipo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, familia imechukua hatua mbalimbali, wamelalamika sehemu mbalimbali, Wajumbe wenzake wa RCC Kigoma tumehoji kwenye vikao, Wajumbe wenzake, Mameya na Wenyeviti wamehoji kwenye ALAT, hakuna maelezo yoyote kutoka Serikalini kuhusiana na jambo hili.

T A A R I F A . . .

MHE. KABWE Z. R. ZITTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niendelee.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi kama wawakilishi wa wananchi wa Kigoma tunalaumiwa kwa nini hatumtetei mwenzetu, mwenzetu yupo wapi toka Julai, miezi tisa leo. Naomba Serikali, Waziri wa TAMISEMI ndio Waziri mwenye Mameya wote, Wenyeviti wote wa Council, leo hii wananchi wa Kata ya Simon Kanguye hawana mwakilishi kwenye Baraza la Madiwani la Kibondo kwa sababu hawajui Diwani wao yupo wapi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mwenyekiti wa Council (Diwani) ni Diwani wa Chama cha Mapinduzi, wala siyo Diwani wa Opposition, mnapoteza mwakilishi wa wananchi na hamna maelezo yoyote. Naomba tupate maelezo haya kutoka Ofisi ya Rais, Utawala Bora ambayo ndio wanasimamia Idara ya Usalama wa Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa zote zipo Kibondo ya mtu aliyekwenda kumchukua tena ameenda kumtoa Ofisi ya Chama cha Mapinduzi, kumpeleka Ofisi ya Mkurugenzi, kumpeleka kwa DSO ambaye alikuwepo kwenye Ofisi ya Mkurugenzi na mpaka leo haonekani. Habari ambazo zinasambazwa Kibondo ni kwamba Mheshimiwa Kanguye tayari ameuawa, tunataka maelezo ya mtu wetu huyu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niseme kitu kimoja na wazee kama Mzee Mkuchika wanisikie vizuri. Sisi watu wa Kigoma ni watu wa Kigoma kwanza kabla ya kuwa Watanzania na naomba hili lieleweke kabisa. Haiwezekani tuonekane siyo raia, viongozi wetu na Madiwani wetu wakamatwe, wapotee na hakuna maelezo yoyote hatutakubali, kamwe hatutakubali na hatushindwi vita. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba kupata maelezo ya Mwenyekiti wa Council ya Kibondo, Simon Kanguye, familia yake inalia kila siku mchana huu nimetoka kuongea na mke wake na wadogo zake, hawana taarifa. Naomba Serikali itupe taarifa yupo wapi Mjumbe mwenzetu wa RCC Kigoma, kama mmemuua mtuambie watu watoe matanga, hatuwezi kuendelea na hali hii. Na ninarudia, watu wa Kigoma, ni watu wa Kigoma kwanza kabla ya kuwa Watanzania na ninaomba lieleweke hili. Kwenye hili watu wa Kigoma, Kakonko, Kibondo, Uvinza na wapi wote tupo pamoja. Mtueleze Mwenyekiti wa Council na Diwani wa Kibondo yupo wapi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ambalo napenda kulichangia, Halmashauri zetu kuna kazi inafanyika na nimesoma hotuba ya Waziri na bahati nzuri Waziri alikuwa Naibu Waziri kwa hiyo alijitahidi, alizunguka maeneo mengi kwa hiyo anafahamu eneo ambalo analifanyia kazi. Tuna tatizo kubwa sana la fedha za maendeleo kutokwenda kwenye Halmashauri zetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwenye taarifa yake aliyoitoa hivi karibuni juzi, ameonesha kwamba asilimia 49 ya fedha zilizotengwa kwenye bajeti ya 2016/2017 hazikufika kwenye Halmashauri zetu. Mwaka jana tumetenga fedha zingine, nimesoma hotuba ya Waziri ukurasa wa saba anaonesha kwamba mpaka Februari fedha ambazo zimefika zote na sasa hivi Mheshimiwa Waziri wa TAMISEMI Selemani itabidi mnisamehe kidogo, mmechakachua hotuba sasa hivi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, siku zote hotuba za Mawaziri zinaonesha fedha za kawaida ngapi zimefika, fedha za maendeleo ngapi zimefika, kwenye hotuba hii ukurasa wa saba mmesema tu kwa ujumla fedha ngapi zimefika, fedha ngapi za maendeleo hazijafika hamjaeleza kwenye hotuba mpaka Februari mwaka huu. Lakini taarifa ya CAG inaonyesha almost 49 percent, nusu ya fedha zinazotengwa kwa maendeleo hazifiki. Sasa tunatunga bajeti kwa ajili ya nini? Kama budget credibility ipo namna hii, kama fedha zinatengwa haziendi tunatunga bajeti kwa ajili ya nini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni muingiliano. Bunge lililopita hapa tulisikia malalamiko ya Tunduma, kwamba Halmashauri haifanyi kazi kabisa Tunduma kwa sababu ya muingiliano kati ya Mkuu wa Wilaya na Madiwani. Pili, kuna muingiliano wa kisiasa vilevile kwenye maeneo kadhaa nchini. Kwa mfano, CAG anasema kwamba Halmashauri hazikusanyi mapato, Halmashauri yangu ni moja ya Halmashauri ambazo zina matatizo ya mapato, hayakusanywi, magumu kupatikana. Halmashauri nyingi sana only 17 percent ya mapato ndiyo imekusanywa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumekaa, tumetunga by- laws, tumeileta Serikalini, Waziri wa TAMISEMI amesaini by-laws, ushuru uanze kukusanywa, anakuja Kiongozi wa CCM Taifa Kigoma anasema kwamba msilipe huo ushuru. Fedha ambayo tumepanga kukusanya ndiyo inalipwa Tabora, ndiyo inalipwa Sumbawanga, ndiyo inalipwa Nzega, ndiyo inalipwa Kasulu, ndiyo inalipwa Kibondo, shilingi 50,000 kwa kizimba, lakini sisi tunakuja kuambiwa msikusanye, hii ni nini hii?

Mheshimiwa Mwenyekiti, watendaji nina barua hapa za mawasiliano kati ya TAMISEMI na Meya wa Halmashauri kuhusiana na namna ambavyo watendaji hawasimamii vizuri fedha za Halmashauri. Halmashauri yangu imepata hati chafu mwaka huu kwa sababu mapendekezo yote ambayo Meya ameyaandika na barua kutoka TAMISEMI, Katibu Mkuu Mhandisi Mussa Iyombe ameandika barua, Naibu Katibu Mkuu Zainab Chaula ameandika barua kuelekeza hatua za kuchukuliwa, hakuna hatua iliyochukuliwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeona hatua imechukuliwa baada ya juzi CAG kutoa taarifa na kusema kwamba watu wasimamishwe, ndiyo tumeona hatua imechukuliwa. Lakini toka mwaka 2016 Meya wa Halmashauri anaandika barua na nitaziweka Mezani hapo Waziri azione, hakuna hatua inayochukuliwa. Sasa mambo haya mtakuja kuwaumiza bure wananchi, kwa sababu wananchi siyo wanaoandika taarifa. Kuna hoja kumi hapa za hati chafu ya Manispaa ya Kigoma Ujiji, kumi. Katika hizo hoja, tisa ni za watendaji, tutawajibuje wananchi, tutafanya nini katika mazingira kama haya? Haya ni matatizo ya viongozi wakubwa kuwapa viburi watendaji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Rais alipokuwa Moshi aliwaambia watendaji, Madiwani wasiwapelekepeleke, wakiwapeleka atavunja Halmashauri. Madiwani wakikaa kwenye Kamati ya Fedha na Uongozi wanatoa maelekezo kwa watendaji hawafanyi, ndiyo barua hizi. Tumepata hati chafu Mheshimiwa Jafo kwa sababu Mkurugenzi hakuchukua taarifa ambayo imefanyiwa marekebisho kumpelekea CAG kwa wakati, mpaka leo anayo ofisini, tunafanya nini? Kwa hiyo, ninaomba haya mambo tuyaangalie upya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la mwisho kabisa ni mapato ya ndani ya Halmashauri. Mapato ya ndani ya Halmashauri yanaathiriwa sana na maamuzi… (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)