Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami nashukuru kwa kupata nafasi ya kuchangia katika Wizara hizi muhimu. Awali ya yote ninapenda kusema mambo mawili nimemuona Mheshimiwa Mwigulu pale Simba tatu Mbeya City moja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ambalo ningependa niliseme katika kazi nyepesi duniani ni kazi ya kukosoa hata kama unatazama mpira ni rahisi sana kusema pale Okwi angefanya hivi au Chirwa angefanya hivi lakini ukiingia mambo yanakuwa ni tofauti kabisa. Kwa hiyo, this is the easiest job in the world! Hawa wenzetu wanapokosoa Waheshimiwa Mawaziri niwatie moyo tu kwa sababu wanafanya easiest job in the world wewe take easy tu chapa kazi kanyaga twende. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo nami kama wenzangu ninapenda kuwashukuru Mawaziri na watendaji katika Wizara hizi, Mheshimiwa Selemani Jafo Waziri wa TAMISEMI, Naibu Mawaziri, Mheshimiwa Gorge Kakunda na Mheshimiwa Josephat Kandege, Waziri wa Utumishi na Utawala Bora, Mheshimiwa George Mkuchika. Pia hata Makatibu Wakuu wa Wizara hizi ukienda pale TAMISEMI kwa Mhandisi Mussa Iyombe au kwa mama yangu Dkt. Zainab Chaula na kwa Dkt. Ndumbaro pale Utumishi bado sijapata nafasi ya kukutana na wale Manaibu wengine. Kiongozi yule anatoka kwenye Kiti anakuja huku anakusikiliza, mnajidiliana mnashauriana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la namana hiyo ndiyo uongozi ni jambo la kupongezwa unashida za wananchi wako wanakusikiliza mnashauriana the way forward. Kwa hiyo, ufanyaji wa kazi wa namna hii mimi niwapongeze. Hii ndiyo namna pekee ya kumuunga Mheshimiwa Rais mkono katika ndoto zake za kuendelea kuisogeza nchi yetu mbele. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya pongezi hizi niseme pia pongezi za jumla kwa Serikali kwa watu wa Mafinga, tunapenda kuishukuru sana Serikali katika masuala ya afya, maji na elimu kwa sababu usipokuwa mtu wa kushukuru maana yake ni kwamba wewe pia hustahili kuwepo kwa maoni yangu. Mpaka sasa tumepokea shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya ujenzi wa jengo la utawala, fedha hizi zitaongeza mzunguko katika Mji wa Mafinga. Mwenye kusomba kokoto mwenye kusomba tofali, mama lishe, wote hawa wanatakuwa ni wanufaika wa fedha hizi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Serikali imetusaidia katika maji nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri wa Maji tuna tanki pale la lita laki tano na sasa tumeanza ujenzi wa tanki lingine la lita milioni moja. Hizi ni hatua changamoto bado zipo, haziwezi kumalizika siku moja lakini ni vizuri kushukuru pale ambapo inastahili kushukuru. Kama haitoshi tuna mradi kule Maduma wa ujenzi wa tanki la lita 100,000 pia tuna mradi kule Bumilainga unaendelea, yote ni kusogeza huduma karibu na wananchi, hata katika elimu tumepata takribani shilingi milioni 500 kwa ajili ya kuboresha miundombinu kwenye shule ya sekondari Changarawe, shule ya msingi Maalum Makalala ambapo Mheshimiwa Jafo ukiwa Naibu Waziri baada ya kutembelea tu immediately tukapata shilingi milioni 100 tukajenga bweni na bado tena tumepata karibuni shilingi milioni 220 kuendelea kuboresha miundombinu katika shule ile. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama vile haitoshi katika afya tumepata shilingi milioni 500 nawashukuru sana Mawaziri, Mheshimiwa Waziri wa Afya tumepata ambulance shughuli zinaendelea, yaani ni kwamba kwa lugha nyingine pamoja na kuwa changamoto hazijaisha unaweza kusema Mafinga mambo ni moto. (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikija kwenye changamoto Mheshimiwa Waziri niwaombe, mlituomba tulete taarifa za miradi viporo kutokana na zile fedha za LDG, sisi tunasubiri pesa zile kwa ajili ya kukamilisha Kituo cha Afya cha Bumilainga, ukamilishaji wa zahanati tatu za Kitelewasi, Kisada na Ulole pamoja na nyumba za watumishi. Pia kukamilisha hostel ya wasichana ya Mnyigumba katika kata ya Lungemba na pia kukamilisha ukarabati wa shule ya msingi Kikombo jumla ni milioni 859 ambazo kama Serikali mliona kwamba tuainishe maeneo ambayo katika kuunga mkono juhudi za wananchi basi, ninyi mtatupa pesa tumalizie miradi viporo. Niombe Serikali kama ni Wizara ya Fedha kama ni TAMISEMI basi fedha hizi tuletewe ili tupate kukamilisha miradi ile ambayo wananchi kwa nguvu zao walikuwa wa kwanza kuianzisha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la TARURA, tunashukuru kwamba Mafinga tumepata fedha milioni 500 tumeboresha kituo cha afya cha Ihongole, lakini tunashida kubwa ya barabara unafikaje katika kituo cha Ihongole. Kati ya mahitaji ya Mafinga kwa ajili ya barabara kwa kweli kama siyo changamoto ya barabara kama nilivyosema, katika mambo mengine kwa jinsi tunavyokwenda mpaka kufika mwaka 2020 Mafinga mambo yatakuwa ni moto.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni fire kabisa. Shida kubwa iko katika barabara, kati ya mahitaji bilioni 8.2 kwa mfano kwaka huu 2018 tumetengewa kutokana na ukomo wa bajeti shilingi milioni 830 hii ni kama asilimia kumi ya bajeti, kwa nini.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana ninasema katika suala la TARURA ndugu zangu hata tukiwa na TARURA kumi, kama hatutabadilisha kanuni ya mgao wa fedha za Mfuko wa Barabara maana yake ni kwamba hatuwezi kupiga hatua yoyote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati shughuli hizi zingine za maendeleo zinaenda ni muhimu sana kuhakikisha kwamba wananchi wanaweza kusafiri kutoka sehemu moja hadi nyingine katika kuhakikisha kwamba mazao yanasafirishwa kwenda sokoni. Kwa mfano, Mafinga katika barabara tulizonazo only asilimia 24 ndiyo zile tunaita good and fair kwamba zinapitika, lakini barabara nyingine kiasi cha takribani kilometa 288 ambayo ni asilimia 88 ya barabara ni za udongo. Kwa mfano, hii barabara ya kutoka Mashine ya Mpunga kwenda mpaka Kituo cha Afya Ihongole kwa kuwa ni ya udongo na ile wanaita average daily traffic ni 4,030 maana yake ni kwamba hata ukitengeneza kila wiki kwa sababu ina traffic kubwa itaharibika tu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suluhisho na ushauri wetu Wabunge tutakapoleta Finance Bill hebu katika hizi fedha pamoja na kazi nzuri ambayo TANROADS wamekwishafanya tupeleke mgao kutoka asilimia 30 mpaka walau asilimia 50, kwa sababu TARURA wenye barabara zaidi ya kilometa laki moja wanapata asilimia 30, TANROADS wenye barabara takribani kilometa 30,000 wanapata asilimia 70 ya fedha. Hata tuwe na TARURA bado wananchi wa Mafinga, wa kutoka Changarawe kwenda kule Mtula ambako kuna irrigation scheme hawataweza kunufaika na ku-feel matunda mema ya Serikali ya Mheshimiwa John Pombe Magufuli. (Makofi)

Kwa hiyo, suluhisho pekee, kwa sababu kazi yetu Wabunge ni kushauri, tushauri kwa pamoja ili kanuni ya mgao wa fedha za barabara iweze kubadilika ili TARURA isibakie kuwa TARURA jina bali iwe TARURA ambayo ina resources za kuweza kufanyia kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kumalizia napenda kuipongeza Serikali, wenzetu wa Mufindi kwa jitihada zetu pamoja na Mheshimiwa Kigola, Mheshimiwa Dada Rose Tweve, Mheshimiwa Mahmoud Mgimwa sasa wanakwenda kupata shilingi 1.5 bilioni ili wawe na hospitali yao na hivyo kupunguza msongamano katika hospitali ya Mafinga. Hata hivyo, kwa kuwa hospitali hii haitajengwa overnight ndiyo maana nasisitiza tupate fedha zile za miradi viporo ili tukamilishe zile zahanati na Vituo vya Afya vya Bumilainga kusudi kupunguza msongamano kwenye Hospitali ya Mafinga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema haya, naunga mkono hoja na Mungu aibariki Mafinga, abariki watu wa Mafinga na aibariki Tanzania kwa ujumla. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.