Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora

Hon. Rehema Juma Migilla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora

MHE. REHEMA J. MIGILLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia nafasi na mimi jioni hii nichangie kuhusu Wizara ya TAMISEMI na Wizara ya Utumishi na Utawala Bora.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niwapongeze Mawaziri wote Wizara hizi mbili, Mheshimiwa Jafo na timu yake Mheshimiwa Kakunda na Mheshimiwa Kandege, lakini vile vile Mheshimiwa Mkuchika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Naanza kuchangia kama ifuatavyo na nianze na suala la elimu. Ni ukweli usiopingika kuwa elimu yetu kwa sasa imedolora na inashuka kiwango siku hadi siku. Hii inatokana na ukweli kwamba nchi yetu imeifanya elimu kama huduma na kuwaandaa watu kuwa ni wa kufaulu mitihani tu na si kwenye uwekezaji. Kama nchi haina kipaumbele kwenye elimu na inaifanya elimu kama huduma obviously hatuwezi kufika mbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaiomba Serikali yetu, kama kweli tunataka elimu yetu ikue naomba sana ijikite kwanza kuifanya elimu ni uwekezaji na badala ya huduma. Vilevile ili elimu hii iweze kuwa na tija kwa hawa vijana ni lazima basi hii mitaala ya elimu ifanyiwe reformation, kwa sababu sasa hivi ukiangalia inawaandaa tu wanafunzi kufaulu mitihani, lakini hakuna ujuzi wowote inayowapatia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii kijana anamaliza darasa la saba, anamaliza form four, anamaliza form six mpaka Chuo Kikuu hana ujuzi wa aina yoyote, matokeo yake kila siku wanatembea na bahasha mitaani mpaka zinapauka. Naiomba Serikali yetu kama kweli tunataka tujikite katika elimu basi haya ninayoyasema, mitaala ifanyiwe reformation na ijikite zaidi katika kuwapa wananfunzi skills ili wahitimu hawa wanapomaliza, kama ni kidato cha nne basi ajue anatoka na ujuzi gani badala ya kuwa anazurura mitaani. Leo hii vijana hata wa chuo kikuu badala ya kuwa ni job creators wamekuwa ni job seekers, naomba hili suala tuliangalie. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi ya ualimu na walimu. Kazi hii ya ualimu inaonekana kama ni kazi ya watu waliofeli, mimi ni mwalimu by profession, inaniuma sana jamii inaiona hii kazi ya ualimu kama ni kazi ya waliofeli. Hii inajidhihirisha unapoangalia kwenye matokeo hata ya form four, division one, division two wanaenda high school, halafu divison three hadi four ndio wanaopelekwa ualimu. Kama tanataka kweli tuwekeze kwa nini hii division one na division two ndio wasipelekwe ualimu? Mpaka jamii inamuona mwalimu ni mtu mjinga mpaka inafikia anaulizwa yaani umekosa hata nafasi ya kwenda kwenye ualimu! Jamani ualimu ni kazi kama zilivyo kazi zingine wote tuliomo humu tumepita kwa mwalimu kwa nini huyu mwalimu leo hathaminiki? Naomba Serikali impe hadhi mwalimu kama inavyompa mtu mwingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwalimu wa Tanzania ana changamoto nyingi sana ambazo zinamkumba. Leo hii walimu wamekosa morali wa kufanya kazi na takwimu zinaonesha wanafanya kazi chini ya kiwango, yote hii inasababishwa na Serikali kwa kutowajali walimu. Walimu wana stahiki nyingi sana ambazo wanazidai lakini Serikali haitekelezi. Wana madeni ya arrears, wana madeni ya nauli, ya nini Serikali haitekelezi. Nataka nijue leo hii Serikali inatumia vigezo gani pindi inapowalipa hawa wafanyakazi au walimu stahiki zao mbalimbali. Kwa mfano katika Jimbo la Tabora mjini kuna hizi shilingi bilioni mia mbili zilizotolewa na Mheshimiwa Rais kwa ajili ya kuwalipa walimu, lakini ni walimu 18 tu ndio wamelipwa wakati kuna idadi kubwa ya walimu hawajalipwa. Sasa nataka TAMISEMI mtuambie ni vigezo gani ambavyo mnavitumia kuwalipa hawa walimu stahiki ili hali wana madeni mengi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niipongeze Serikali kwa kuanzisha elimu bure, elimu bure inaende sambasamba na kutoa posho kwa walimu wakuu wakuu wa shule na waratibu wa elimu kata. Hata hivyo ndugu walimu wana mishahara midogo sana. Tunaomba basi katika hii posho mnayowapa walimu sijui wakuu wa shule ma-headmaster na waratibu wa elimu kata basi na walimu na wenyewe wapewe hata kidogo, kwa sababu hawa wakuu wa shule mnaowapa pesa hawafanyi kazi peke yao wanafanya kazi na walimu wengine, nao tunaomba muwape hata kidogo kama motisha ya kuweza kufanya kazi vizuri na kwa ufanisi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine nizungumzie mchakato wa kuhamisha walimu wa sekondari wa arts na kuwapeleka primary. Mheshimiwa Haonga amesema ni ukweli usiopingika ni wazo zuri, lakini approach inayotumika sio nzuri. Walimu hawa walivyokuwa wanasoma kwenye vyuo vyao walisomea masomo mawili, leo hii unawaambia wakafundishe kule watafundisha kitu gani? Mbaya zaidi hakuna hata induction course ambayo mmewaandalia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaiomba Serikali basi angalau iwape induction course hawa walimu ili waweze kwenda kufundisha kwenye mazingira yale. Tukumbuke kwamba walimu hawa wamekuwa trained kufundisha wanafunzi wenye kimo kikubwa, leo wakafundishe watoto wadogo wataweza? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, bado njia za ufundishaji watoto wa sekondari ni tofauti na watoto wa primary. Kwa hiyo, tunaiomba Serikali yetu kama kweli tunadhamiria kuinua kiwango hiki cha elimu, japokuwa ni approach, nzuri basi hawa walimu wapatiwe induction course angalau ya mwezi hata mmoja kwenye methodologies. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine nizungumzie hii Tume Utumishi wa Walimu. Tume hii inafanya kazi kubwa sana na naiomba Serikali iiongezee pesa ili iweze kufanya kazi yake kwa uhakika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niende kwenye kazi nyingine ambayo inafanywa na Wizara ya TAMISEMI. Kazi moja wapo ni kuhakikisha inatatua migogoro inayotokana na ardhi. Mkoa wa Tabora hususani Manispaa ya Tabora walikumbwa na bomoa bomoa, watu hawa walijenga katika maeneo ambayo walipewa kisheria na bado Serikali yetu ikaweka hadi miundombinu kule na bado walikuwa wanachukua hadi kodi lakini leo hii hawa watu wanaambiwa wahame lile eneo ilhali walipimiwa na Serikali na wako pale kisheria lakini hatuoni dalili zozote za kupewa fidia au kutafutiwa eneo jingine. Naiomba sana Serikali iwanusuru watu hawa, tunaomba basi watu hawa wapatiwe eneo jingine au wapewe fidia waweze kuanza maisha mengine mapya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni katika uwezeshaji wa vikundi vya wanawake na vijana, ile asilimia 10 ya mapato ya ndani. Hizi asilimia zipo kisheria lakini halmashauri zimekuwa hazitengi pesa kwa ajili ya kuwapatia vijana, hali inayopelekea vijana sasa hivi wafanye kazi ambazo ni tofauti na ndoto zao. Tunajua kabisa kila mmoja ana kazi ya ndoto yake, lakini vijana wengi sasa hivi wanafanya kazi ya kuendesha boda boda, wanawake wengi wamekuwa bar maid ni kazi ambazo ziko nje ya ndoto zao. Kama Serikali itahimiza halmashauri kutenga asilimia 10 vijana hawa watanufaika na wataacha kuhangaika huko mitaani. Tunaiomba Serikali hizi halmashauri zisizipe mzigo mkubwa yaani mapato yarudi kule kwenye Serikali za mitaa badala ya kwenda Serikali Kuu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala jingine ni kuhusu utumishi. Tulipiga kelele sana kuhusu watumishi wa darasa la saba. Ni kweli kabisa watumishi hawa waliajiriwa na Serikali na Serikali hii ndio tena ikawatoa kazini, lakini Serikali hii tena imewarudisha kazini, ni jambo zuri na wazo zuri, lakini suala langu ni hili, je, Wizara ina mpango gani au itawalipa kwa fungu lipi watu ambao hawajafanya kazi kwa muda mrefu sana? Pia kuna watu ambao tayari walishaajiriwa ku-cover hizi nafasi za watu walioko darasa la saba, je, hawa watu ambao sasa wameshaajiriwa kuziba zile nafasi za watu wa darasa la saba watatolewa kazini au vipi? Naomba majibu.