Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Mariamu Ditopile Mzuzuri

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. MARIAM D. MZUZURI: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehma mwenye kurehemu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, napenda kukushukuru wewe, Mheshimiwa mtani wangu, maana niliona mbona napitwa, muda unazidi kwenda na mimi sipati nafasi. Napenda ni-declare interest, mimi ni mkulima. Tumezoea kusikia mtoto wa mkulima, mtoto wa mfugaji, mimi ni mtoto wa kishua, lakini ni mkulima. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuanza kwa kusema, naipongeza Tanzania, napongeza Serikali zote za Chama cha Mapinduzi kuanzia Awamu ya Kwanza, ya Pili, ya Tatu, ya Nne na hii ya Tano.
Waheshimiwa Wabunge wenzangu, huu mchezo hauhitaji hasira na msema ukweli mpenzi wa Mungu. Kama wewe unasema tupo nyuma, India wanatambua korosho bora inapatikana Tanzania, dunia inatambua mwaka 2015 kwa mujibu wa FAO kati ya nchi 10 duniani zinazoongoza kwa kuzalisha ndizi, Tanzania imo. Pamoja na yote, tumo kwenye ramani. Serikali zetu zimekuwa zikihangaika na kilimo na zinazidi kuboresha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Rais, ametuletea wahusika ambao watatuvusha. Nina uhakika kipindi hiki cha 2015 na ninamwomba Mheshimiwa Rais, hii timu wasiibadilishe mpaka tufike 2025; Mheshimiwa Mwigulu na mwenzake watatuvusha mbali sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, yapo mambo ya kuyaboresha ili tufike mbali. Cha kwanza ni sera, kwa sababu kuna vitu tunashangaa tu. Leo hii haiwezekani mbegu inayozalishwa hapa nchini iwe inatozwa ushuru mkubwa kuliko mbegu inayoagizwa kutoka nje. Kwa sababu wataalam wanasema, mbegu inatakiwa ifanyiwe tafiti mahali husika. Kuna factors nyingi za hali ya hewa na aina ya udongo uliopo. Kwa hiyo, tukibadilisha hizi sera zetu, namwomba Mheshimiwa Waziri akae chini apitie sera zilizopo, je, zinaendena na wakati? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hizi zitamsaidia yeye maana kuna watu wameshaanza kumtisha, na mimi nikakumbuka, ametaja baadhi ya Mawaziri ambao walipitia Wizara yako leo hii hawajarudi, nikakumbuka na baba yangu mdogo yumo kipenzi changu Mheshimiwa Adam Malima, na yeye alipita huko hajarudi, lakini nasema kwamba Mheshimiwa Mwigulu utaiweza na itakufikisha sehemu ambapo wewe unapaota, angalia hizi sera! (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna jambo moja limechangiwa sana na watu hapa, mimi ni mwana maendeleo, ni kijana, ninalinda interest ya kundi kubwa ambalo lina-constitute hii nchi. Kuna watu mnawasema vibaya, jamani wafanyabiashara wamo humu, kuna biashara ambayo haina channel of distribution? Kwenye biashara lazima una producer, una mtu wa katikati ambaye anapeleka kwa final consumer. Kwa nini kwenye kilimo huyu mtu wa kati anapigwa sana vita? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niliomba ridhaa kwa Wana-Dodoma hususan vijana kuja kuwawakilisha, mimi mkisema hivyo mnaniumiza. Nina vijana wengi sana ambao wanafanya biashara za mazao na naomba kuwasemea, wanafanya kazi kubwa kuisaidia Serikali kuendesha kilimo. Hawa watu wana-invest kule. Ninyi mnapochelewa kupeleka mbegu, hawa ndio wanaenda kuwapa wakulima mbegu na muda mwingine inaweza kutokea mvua hazijatosha, hawajapata kitu. Hela zao wao ndio zinakuwa zimepotea.
Naomba tuwaendeleze hawa, tuone ni namna gani ya kuimarisha mahusiano baina ya wakulima na hawa vijana wetu. Haiwezekani leo hii tumsifie kijana Mtanzania anayeenda kuchukua nguo China kuja kuuza, tumkandamize huyu ambaye aliamua kufanya kazi na mkulima. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, yapo mambo mengi, nimeshauri sana tangu niwe Mbunge kwa sababu nina interest na kilimo na ninajua kilimo ndiyo cha kututoa.
Napenda kuzungumzia vijana. Kuna kundi moja la vijana ambao ni wahitimu wa Vyuo Vikuu, imekuwa kwao tatizo ni ajira, lakini wapo ambao wanajitolea, mmojawapo ni mimi. Tangu nilipomaliza diploma niliamua kuingia kwenye kilimo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaelekea kwenye uchumi wa viwanda, lakini hawa vijana kutumia vile vyeti vyao tu kama collateral na Serikali iwasimamie vizuri, waweze kuwezeshwa kufanya kilimo chenye tija na cha biashara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, unaweza ukaunda kundi la hawa wahitimu mmoja akiwa mtaalam kutoka SUA mwingine awe accountant, mwingine awe mtu wa procurement, mwingine awe marketing; wakiungana hao wakaenda shambani na ukawawezesha kwa nyenzo, wakaenda kulima, wakauza, watafanikiwa na wao wenyewe watakuwa ni source ya ajira kwa vijana wengine. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nina mambo mengi sana ya kuchangia, nitaandika kwenye mchango wa maandishi. Tunataka kumtoa Mtanzania kwenye kilimo cha jembe, Mheshimiwa Mwigulu thubutu na utaweza. Weka sera ya kila kijiji kiwe na trekta. Tuna vijiji 19,200 kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2012; ukipiga hesabu ya trekta moja farm track ya milioni 35 na hiyo ni bei ya hapa Tanzania, inakuja hesabu ya kama shilingi bilioni 600.7. Ukithubutu utaweza kwa awamu, sio vijiji vyote vitahitaji! Utaweza na utakuwa umeacha trade mark ambayo haitafutika mioyoni mwa Watanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri, kwa kuwa tunataka tuweke uchumi wa viwanda, tufanye kilimo cha biashara. Naomba tuanzishe agricultural zones, ifahamike. Ukanda ambao unalima ndizi, u-concetrate, uboreshe mbegu nzuri za ndizi ambazo tutaweza ku-export. Tunaweza kwenda Bukoba na Mbeya hawa wakawa zones za kulima ndizi, machungwa kwa watani zangu Tanga, mananasi kwa watani zangu Wasukuma Geita, pamoja na kwa kaka yangu Mheshimiwa Ridhiwani, ikawa ni zone kwa ajili ya mananasi. Tuna kilimo cha maua, leo hii Songwe, Mbeya, Iringa Arusha na uzuri miundombinu ipo, kuna airport, we can export fresh flowers to Europe and elsewhere in the world. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikirudi kwetu Kanda ya Kati tukazanie kwenye alizeti, ufuta, choroko, dengu, mbaazi and I tell you Tanzania ni nchi ya tatu katika Afrika ku-produce mbaazi. Tunatengeneza mbaazi nzuri kweli! Mpwapwa kwa Mzee Lubeleje ndio wanatengeneza the best karanga in the world ambayo inatoa mafuta mazuri. Kwa nini tusitumie fursa hii kwa ajili ya kupata kipato kikubwa katika nchi yetu?
MHE. MARIAM D. MZUZURI: Kwa hiyo, nashukuru sana. Naunga mkono hoja.