Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Wilfred Muganyizi Lwakatare

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Bukoba Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. WILFRED M. LWAKATARE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.

Kwanza niseme kabisa natambua Jimbo langu la Bukoba Mjini pamoja na pale Kyerwa angalau kupewa fedha za kupanua hospitali yetu 1.5 billion shillings, inabidi nitambue hilo na ninalipongeza. Najua hatua hii itapunguza idadi kubwa ya wagonjwa ambao wanatibiwa kwenye Hospitali ya Rufaa pale Bukoba Mjini, sasa angalau itapatikana alternative.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, kwenye ukurasa wa 103 kifungu namba 179 cha hotuba ya Mheshimiwa Waziri, amezungumzia huduma na malezi kwa ajili ya watoto wachanga na zile care centres. Sasa niseme, lipo tatizo la vituo hivi na siyo kwa Jimbo langu, nafikiri ni kwa Tanzania nzima, kwa utaratibu uliopo hivi sasa na kwa Bukoba Town, ni kwamba wale Maafisa wa Ustawi wa Jamii walitoa barua ambayo ilivifunga vile vituo. Ile barua kwa sababu waliandika kwa shinikizo baada ya kutiwa ndani na vyombo vya dola, waliamua vituo vifungwe siku hiyo hiyo wakati waliposhinikizwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa wakati wakivifunga wanarejea sheria ambayo kimsingi ipo, kwamba ili kufungua hizi centres lazima uwe umepata usajili kutoka kwa Kamishna. Tunatambua hiyo sheria, ipo, je, ni kweli inaendana na mazingira halisi ya hivi sasa na watoto tulionao?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimemsikia Waziri katika hotuba yake ametoa takwimu za vituo vilivyopo kwamba mwaka 2017/2018 wamesajili vituo 139; mwaka 2016/2017 vilisajiliwa vituo 270 na hadi sasa viko vituo 1,046 kwa Tanzania nzima. Sasa hii hali haiendani na ukweli kutokana na nini kinachoendelea katika mazingira yetu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nieleze kwa ufupi. Ni kwamba vituo hivi kwa mujibu wa sheria ili visajiliwe inabidi viwe na walezi wasiopungua 20; mlezi mmoja kwa ratio ya watoto 20, kuwe na first aid kit, kuwe na fire extinguisher, kuwe na vyoo vya mashimo matatu, kuwe na jiko la kupikia uji, kuwe na uzio uliozungushwa kwenye kituo kizima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakubali kwamba sheria hii inaweza ika-apply Oysterbay au Mikocheni, lakini kwa mwananchi ambaye yuko Katatolowanzi Bukoba Town, aliyeko Kaororo, aliyeko Nshambia, mimi nasema hiki kitu hakiwezi ku-apply kwa sababu hakiendani na mazingira ya wananchi wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwamba pamoja na sheria hii, iko sheria inayotambua kabisa kwamba kwenye sehemu ya 12, kwenye masharti mengineyo, kifungu cha 155 kinatambua kwamba Mamlaka ya Serikali za Mitaa inaweza kushauriana na Waziri wa masuala ya Ustawi wa Jamii kutoa sheria ndogo ya miongozo kwa kuzingatia mazingira ya eneo lenyewe, lakini maafisa wetu wamekuwa hawajikiti katika masharti haya, wao wanafunga vituo kwa kutegemea kwamba vyote visajiliwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri, nataka kutamka tena kwamba jambo hili kwa size ya nchi yetu na kwa jinsi mwamko ulivyopatikana kwa watu kuanzisha vituo vyao kwa maeneo mbalimbali, hata kwenye Kijiji cha Nkasi vituo vinafunguliwa…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)