Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Joseph Leonard Haule

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mikumi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. JOSEPH L. HAULE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuchangia kwa dakika hizi tano ulizonipa katika Wizara hii nyeti Wizara muhimu sana kwa maisha ya Watanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Wizara hii tumeona kuna changamoto kubwa sana za miradi mbalimbali kuweza kufika kwa wakati katika maeneo ambayo yanastahili.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ni-declare interest, mimi ni Mjumbe wa Kamati ya Huduma na Maendeleo ya Jamii. Kitu kikubwa ambacho naweza nikakizungumza kwa haraka, baada ya lile zoezi la kutumbua wafanyakazi wa vyeti fake, tumekuwa na athari kubwa sana ya watumishi katika maeneo yetu hasa Mkoa wa Morogoro. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa Wilaya yetu ya Kilosa uhitaji wa watumishi ulikuwa ni 1,025 kwenye kada mbalimbali kama Wauguzi, Madaktari, Wafamasia, Ustawi wa Jamii na Maafisa Afya, lakini waliopo ni 474 tu, sawa na asilimia 46. Pia tuna upungufu wa watumishi 551 sawa na asilimia 54. Unaweza ukaona jinsi ambavyo Wilaya ya Kilosa imekuwa nyuma sana katika sekta hii ya afya na watu wamekuwa wakitaabika sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wito wangu kwa Serikali, tunaomba itusaidie sana watumishi hawa waweze kufika katika Wilaya yetu ya Kilosa lakini pia tuweze kuokoa maisha ya mama na mtoto ukizingatia jiografia ya Wilaya ya Kilosa imekuwa iko mbali mbali sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, kiukweli kabisa tumeona kwamba kuna upungufu mkubwa wa vituo vya afya ambapo sasa hivi Serikali imetoa shilingi milioni 400 pale kwenye Kituo cha Afya cha Kidodi, tunashukuru sana. Pia kituo hiki ni muhimu kwa sababu kinaenda kuhudumia wananchi wa Kata ya Ruaha, Vidunda, Kidodi pamoja na Rwembe. Kwa jiografia iliyoko pale tunaona pia kuna umuhimu wa kusisitiza na kuiomba Serikali iweze kutupatia gari ili liweze kusaidia wananchi wa Jimbo la Mikumi.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika upungufu huu wa Madaktari Bingwa katika Wilaya yetu ya Kilosa, mwaka 2017 tulisikia Serikali inataka kupeleka Kenya Madaktari 500, basi kwa upungufu huu tunadhani mngetudondoshea pale Mikumi kidogo Madaktari Bingwa kadhaa ili waweze kutusaidia katika Wilaya yetu ya Kilosa, hii ingeweza kusaidia sana. Pia dawa zimekuwa zinafika chini ya kiwango; dawa zimekuwa chache. Unaposikia kuna shilingi trilioni 1.5 hazieleweki zimekwenda wapi kwa kueleweka, nadhani zingeweza kuwa zimepangiwa mkakati maalum katika kitengo hiki cha afya na kuweza kuwasaidia mama na mtoto, tungeweza kupata hesabu nzuri sana na Serikali ingeweza kutimiza malengo ya kuwasaidia Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia kuna kitu ambacho Serikali inabidi iongeze nguvu. Katika Maafisa Maendeleo wa Jamii wamekuwa pungufu sana. Kwa nchi nzima tunaona kwamba uhitaji ni watumishi 4,000 lakini waliopo ni 1,700. Kwa hiyo, unaona kwamba asilimia 57.5 kuna upungufu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Maafisa Maendeleo ya Jamii ndiyo wahamasishaji wakubwa katika Wilaya zetu, katika maeneo yetu kuwahamasisha wananchi waweze kujiletea maendeleo yao. Unapokuwa huongezi msisitizo katika kada hii na kufanya upungufu katika watumishi wa Maafisa Maendeleo ya Jamii inakuwa inashindwa kuwa-connect Watanzania na wananchi katika kujiletea maendeleo yao katika maeneo yao. Kwa hiyo, naiomba sana Serikali iongeze nguvu katika kuongeza Maafisa Maendeleo ya Jamii. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vyuo tumevitembelea, bajeti haziendi kwa wakati na vyuo vimekuwa katika hali mbaya. Namuomba sana dada yangu, Mheshimiwa Ummy, waongeze nguvu kwa kuongeza Maafisa Maendeleo ya Jamii ili waweze kuwa chachu na kuwakusanya wananchi pamoja, waweze kujadiliana nao ili kujiletea maendeleo katika maeneo yao. Maana huwezi ukaongelea maendeleo katika Jimbo, Wilaya na katika Mkoa bila kuwahusisha Maendeleo ya Jamii. Hao ndio wanaoweza ku-connect Serikali na wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tunapokuja kuongelea suala la barabara, suala la wananchi kulima, watu kufanya programu mbalimbali katika nchi yetu, Maafisa Maendeleo ya Jamii ni watu wa muhimu sana. Naiomba sana Serikali iongeze nguvu zake katika kuajiri watu hawa. Asilimia 57, unaweza ukaona upungufu huo ni mkubwa sana na inatia damage kubwa sana kwa Serikali.

heshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.