Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Eng. James Fransis Mbatia

Sex

Male

Party

NCCR-Mageuzi

Constituent

Vunjo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. JAMES F. MBATIA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Ninaamini nina dakika kumi za kuchangia.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipatia nafasi hii. Kwanza kabisa nianze na maswali kwa Mheshimiwa Waziri.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka kujua tu, Serikali uwekezaji wake katika sekta ya afya ni asilimia ngapi? Sekta binafsi uwekezaji wake katika afya kwa ujumla wake ni kiasi gani na ndani ya sekta binafsi, mashirika ya dini yanachangia huduma ya afya kwa kiasi gani? Ni kiasi gani kuna ubia kati ya Serikali na sekta binafsi? Kuna ubia kiasi gani kati ya mashirika ya dini na Serikali? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nasema hivyo kwa sababu lengo la nne la Malengo Endelevu ya Dunia inazungumzia afya bora kwa wote ifikapo mwaka 2030. Nawapongeza wataalam wetu katika sekta ya afya, Waziri, Katibu Mkuu Dkt. Mpoki, wataalam; akina Profesa Mseru, akina Dkt. Janabi na wenzao, KCMC, Bugando na wote. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tuwe wakweli tu, katika Taifa letu, sekta ya afya japo wanafanya kazi kubwa na juhudi kubwa hatujawawezesha sekta hii kibajeti waweze wakatekeleza majukumu yao inavyotakiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kama Serikali yetu iko kwenye hali hii, basi inabidi kuweka vivutio rafiki, mazingira rafiki, hata tukaangalia motisha kwa sekta binafsi tuweze kupata wawekezaji wakubwa wanaoaminika waweze wakasaidiana na Serikali katika sekta ya afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimejaribu kufanya utafiti nimeona ni Aga Khan peke yake ambayo imeweza kuwekeza zaidi ya shilingi bilioni 200 kwa sasa kwenye sekta ya afya.

Wako wapi wawekezaji wakubwa kama Aga Khan wawekeze ili afya ya Mtanzania, utu wa Mtanzania ukaweza kupata nafasi yake? Duniani kukoje, nikiangalia namna gani tunaweza tukafanya a medical tourism katika maeneo fulani hapa Tanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi natoka Vunjo, pale Vunjo tuna Hospitali ya Kilema ya Kanisa Katoliki, ubia na Serikali; tuna Hospitali ya Marangu ya KKKT; Kirueni wanaanzisha hospitali yao kule Mwika ambapo wana vifaa vya kisasa; wana MRI na CT Scan, lakini hawana majengo ya kutosha. Vifaa hivi wamepata Canada, Serikali ishirikiane nao ili hata watu waweze kutoka nje kuja kutibiwa Tanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, pale kuna kupanda Mlima Kilimanjaro; hali ya uokoaji wa wapanda Mlima Kilimanjaro, miundombinu rafiki tunaifanyaje? KCMC iko pale, tunatokaje ndani ya box ili tuweze kusema eneo fulani tunatengeneza a medical tourism na facilities za kutosha zipo na tukaacha ku-export au kwenda kutafuta huduma za afya nje ya Watanzania? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nasema hayo kwa sababu ukiangalia huduma zinazotolewa hapa kwetu Tanzania, na mimi ni mhanga, Mheshimiwa Waziri unajua hilo. Ni kwamba inabidi tujitoe na tufikiri kwa mapana kwamba namna gani uhai wa mwanadamu; nimesoma kitabu cha Biblia Takatifu leo asubuhi Yoshua bin Sira ule mstari wa 16:30 inasema: “Hakuna utajiri ulio bora kuliko afya ya mwili na hakuna furaha iliyo bora kuliko furaha moyoni.” (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tukiangalia Tanzania leo hii tumewekwa wapi kwenye happiness index? Tumewekwa pamoja na Yemen, Syria na Burundi. Tumeshika nafasi ya 153 kati ya nchi 156. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa lazima tutoke tufikiri kwamba kwa nini hatuna furaha moyoni kwenye mambo ya ustawi na kwenye afya zetu? Tukiangalia, Watanzania ni wagonjwa kiasi gani kwenye utafiti? Wataalam wetu tunawasaidia kiasi gani? Kama huyu ni daktari, unamwezesha namna gani? On call allowance, risk allowance, huduma nyinginezo ambazo madaktari wetu hawazipati, waka-concentrate kwenye kutibu tu na masomo yao ya sayansi yalivyo magumu? Unakuta daktari wetu huyu anafuga kuku, huyu ana bar, huyu anaenda kutafuta income nyingine. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ni namna gani tunawaheshimu madaktari wetu? Kwa mfano, daktari ana kitambulisho chake, akipita polisi anamsimamisha, umeongeza speed, amwambie ninawahi kwenda kutibu, polisi anamwachia. Huwezi ukamweka daktari kwenye kundi moja na walevi. You cannot do things like that. (Makofi)

Mjeshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, lazima tufikiri kwa mapana, ni namna gani tunawapa incentives madaktari wetu waweze kufanya research. Wizara yako inatuonesha, kuna upungufu wa wataalam zaidi ya asilimia 50 katika sekta ya afya. Wauguzi, Manesi, Madaktari wenyewe, Madaktari Bingwa na kwingineko. Namna gani tunafanya in training na out training? Nitoe mfano, think globally.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwezi uliopita nilikuwa Zydus Hospital; imeajiri watu wauguzi wake pamoja na madaktari zaidi ya 1,200; lakini wanaotibiwa pale kila siku, wanaoingia na kutoka pamoja na waliolazwa na madaktari wote kwa pamoja ni zaidi ya watu 5,000 kwa siku. Ni shirika kubwa ambalo limewekeza kweli kweli. Serikali ya India imeshirikiana nao namna ya kutoa huduma iliyo bora.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano, kuna mtaalam mmoja anaitwa Dkt. Daria Singh, anaweza akafanya operesheni nne kwa siku moja ya knee replacement na accuracy asilimia 100. Anafanyaje? Ni kwamba huyu amewezeshwa vizuri, amefikiri vizuri, anajua kazi yake anaifanyaje. Sasa hebu tujiulize hapa kwetu, kulikoni? Kuna nini? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa ni vyema Mheshimiwa Waziri tukafanya in training na out training, yaani tukaomba wataalam kama hawa wa Zydus Hospital wakaja kutusaidia kufundisha humu ndani, na sisi tukaenda tukasoma kule kwao. Wataalam wetu tukafanya programu ambazo ni exchange program na tukaweka mazingira yaliyo rafiki. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tuje kwenye vitendea kazi. Kwa mfano, Waheshimiwa Wabunge hapa leo hii wanazungumzia X-Ray kwenye mikoa. Kweli hii ni karne ya kuzungumzia X-Ray, CT Scan na MRI? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tulizungumzia na Serikali imeahidi miaka nenda rudi kuhusu linear accelerator kwa ajili ya wagonjwa wa kansa; mpaka leo hii hakuna linear accelerator nchi hii. Tulikuwa tunamsifia sana Dkt. Janabi na wenzake hapa, mambo ya Cardiac Cath. Lab.; Tanzania tunazo tatu tu, ambapo tuna population ya watu zaidi ya milioni 50 compared na wenzetu wa Kenya wanazo Cardiac Cath. Lab. zaidi ya tisa. Wako kwenye hali bora kuliko sisi katika mazingira haya.

Mheshimiwa Naibu Spika, ukimsoma Yoshua bin Sira sura ya 30:17 inasema: “Afadhali kifo kuliko maisha ya taabu na pumziko la milele kuliko ugonjwa wa kudumu.” Ukijaribu kuangalia ni kwa nini anasema hivi?

Mheshimiwa Naibu Spika, tujiulize kweli afya zetu, ilivyotokea kikombe cha kwa babu kinatibu, karibu nusu ya Serikali yote ilikimbilia kwa babu kwa sababu unaweza kuona afya yako siyo nzuri. Sasa tunafanyaje? Miundombinu ile tuliyopeleka kule, tunaiwezeshaje sekta hii ya afya ili afya za Watanzania ziwe bora? Tuwe wakweli kwamba afya za Watanzania ziko hoi bin taabani. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Bima ya Afya hospitali nyingine zinakataa, hasa hospitali za watu binafsi kwa sababu haitoshelezi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nayapongeza sana mashirika ya dini. Niwe mkweli kabisa! Nawapongeza sana KKKT, Wakatoliki pamoja na BAKWATA kwa kazi nzuri wanayofanya katika kuwekeza kwenye sekta ya afya. Sasa tuwape lugha nzuri, tushirikiane nao vizuri; wao wana mtandao mkubwa duniani waweze kuleta ile technology na ile misaada tukashirikiana kwa pamoja, kwa kuwa dunia yetu hii ni kijiji.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba chonde chonde, inaonesha hata kwenye kitabu chako na kitabu cha Kamati kuhusu lishe, hali ya Tanzania lishe siyo nzuri. Hili tatizo la lishe lilianza tangu miaka ya 1978 pale...

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. JAMES F. MBATIA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana na ahsante sana.