Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Zainabu Nuhu Mwamwindi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. ZAINABU N. MWAMWINDI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nianze kwa kukushukuru wewe mwenyewe kwa kunipa nafasi na mimi leo niweze kuchangia hotuba hii ya Waziri wa Afya, Wizara nyeti, Wizara ambayo kwa kweli imeshika uhai wa Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niungane na Wabunge wenzangu kwa kumpongeza sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa namna ambavyo amejitoa muhanga kwa ajili ya Watanzania. Pia nimpongeze mama yetu Mama Samia Suluhu na yeye kwa kumsaidia kwa nafasi yake ya Makamu wa Rais. Nimpongeze Mheshimiwa Waziri Mkuu na Mawaziri na Naibu Mawaziri wote kwa namna ambavyo kwa kweli wanafanya kazi na macho yetu yanaona na masikio tunasikia yale ambayo wamekuwa wanayafanya katika maeneo yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa namna ya pekee sana ninaomba nimpongeze sana mwanangu Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana Mheshimiwa Ummy Mwalimu na kweli wewe ni mwalimu, lakini niseme tu nitakuwa sijajitendea haki kama sitakupongeza kwa namna ambavyo kwa kweli umethubutu katika Wizara hii kama mama. Niseme tu kweli kwamba hujatuangusha sisi wanawake wenzio na tunazidi kukutia nguvu kwamba changamoto za kawaida kama binadamu na pale unapokosea Mungu anaona kwamba umekosea kwa bahati mbaya lakini nia na dhamira yako ya kweli katika nafasi hii tunaiona na tuseme tu Mheshimiwa Rais hajakosea kukupa nafasi. Pia nimpongeze Naibu Waziri na pia niwapongeze watendaji wote wa Wizara yako. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwa kuunga mkono hoja asilimia mia kwa mia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mpango wa Maendeleo wa Afya ya Msingi (MMAM) ni mpango ambao umeelekezwa na Serikali kwamba kila kijiji kiwe na zahanati, kila kata iwe na kituo cha afya na kila Wilaya iwe na Hospitali ya Wilaya. Zahanati ya Kalenga kwa yeyote ambaye ameshafika Kalenga, na kwa namna ninavyoifahamu Kalenga zahanati ile ni kongwe, imejengwa kabla ya uhuru na haikujengwa purposely kwamba iwe zahanati kwa ajili ya kutoa huduma ya afya, ilikuwa ni shule ya msingi ambayo mimi kwa umri wangu nimesoma darasa la kwanza mpaka la nne, halafu shule ile ikahamishiwa baada ya Serikali kufuta shule za middle school ikahamia kwenye shule iliyokuwa inaitwa Kalenga Upper Primary School na ikawa zahanati ya kijiji cha Kalenga.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kalenga ni kijiji ambacho kina historia na ni kijiji ambacho viongozi wetu wakuu akiwemo aliyekuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Chifu Adam Sapi Mkwawa amezaliwa pale na amezikwa pale, lakini pia ni kijiji ambacho kina makumbusho ya Taifa letu. Kijiji kile kwa sasa ni kijiji mji na idadi iliyokuwepo wakati ule na sasa, idadi ya watu imeongezeka kuliko mara tano. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, zahanati ile kwanza majengo yake yalifanya kuchapiwa tu, kubadilishwa iwe zahanati lakini haina sifa wala hadhi ya kuitwa zahanati ya kijiji cha Kalenga. Kwa sababu dakika tano kwangu ni chache, mengine nitatoa kwa maandishi, nikuombe Mheshimiwa Waziri mwanangu Ummy ushirikiane na Wizara ya TAMISEMI angalau uitazame kwa jicho la huruma, wananchi wa Kalenga wana utayari wa kujenga kituo cha afya, wana eneo lao ambalo limezidi ekari 12 ambalo halina gharama ya Serikali kulipa fidia lakini pia wapo tayari wao kama wao kutumia nguvu zao kuweza kusimamisha kuanza kujenga pia wanaomba serikali pale watakapokwama iweze kuwasaidia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa namna ya pekee sana katika Majimbo magumu ambayo ninayafahamu mimi ni Jimbo la Kilolo. Jimbo la Kilolo kuna shida, wao kutokana na miundombinu ya kwao pale wamekubaliana katika kila kata, vijiji vitatu viunganike vijenge kituo cha afya kimoja.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niunge mkono hoja.