Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Hawa Mchafu Chakoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. HAWA M. CHAKOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuchangia hotuba ya Mheshimiwa Waziri wa Afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, nitaanza kwa kuipongeza Serikali ya Awamu ya Tano lakini pia kumpongeza Mheshimiwa Waziri na Naibu wake kwa kazi nzuri ambayo wanaifanya. Kiukweli Wizara hii ya Afya ina mambo mengi sana na wenzetu Waziri na Naibu wake wanafanya kazi kubwa sana, lakini mwisho wa siku tukubaliane tu hizi changamoto za afya hazitakaa zije ziishe kwa ukamilifu wake, hata zikiisha bado zitazaliwa zingine kutokana na vyakula tunayokula, life style tunayoishi na mabadaliko ya tabianchi. Kwa hiyo, kila siku kwenye Wizara ya Afya changamoto zitakuwepo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa dakika ni tano itoshe kuwapongeza wenzetu kwa kazi nzuri wanayoifanya Serikali ya Awamu ya Tano hasa kwa kujitahidi ama kuweza kuokoa fedha kwa wagonjwa walikuwa wanaenda kupata matibabu ya moyo nje ya nchi. Ukiangalia hapa kwenye hotuba ya Mheshimiwa Waziri inasema wameweza kupunguza ilikuwa kutoka wagonjwa 43 mpaka wagonjwa 12 kwa mwaka 2016/2017; hiyo ni pongezi kubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kingine ninachopenda kuwapongeza kwa lile la kuanzisha chanjo ya saratani kwa mabinti wa miaka 14, wamefanya kazi kubwa sana. Pengine hapa nataka niiombe Serikali yangu iangalie sasa mabinti above 14 yaani huo umri wa wao ambao wameuchukua sasa wanaozidi umri huo, Serikali ina mkakati nao gani? Nilikuwa tu napenda kusaidiwa katika hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kingine ambacho ningependa kukizungumzia kwenye dakika hizi tano, napenda kuiomba Serikali na niliwahi kuuliza swali juu ya sera ya matibabu bure kwa wajawazito, hili bado naliona kama kidogo tuna changamoto nalo, pengine Serikali sasa ione namna bora ya kufanya mapitio upya ya hii sera, kama itabidi vipo baadhi ya vitu tutahitajika kuvitolea ufafanuzi. Hivi bure kwa wajawazito kwenye kila kitu au kuna baadhi ya vitu bure na kuna baadhi ya vitu vingine wananchi inabidi wachangie?

Mheshimiwa Naibu Spika, ni vema hii tungeiweka vizuri kwa sababu hofu yangu wapiga kura na wananchi wetu wengi wanalalamikia kwamba once wako wajawazito wanapoenda hospitalini wanatozwa ama kuwa-charged. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nitoe tu mfano, vidoge vile vya uchungu wanaviita ama dripu, yenyewe ile, nikijitolea mfano hata mimi mwenyewe binafsi, nililipia kwa cash ingawaje nina kadi ya NHIF ni kadi ya Bunge ambayo naamini katika kadi ambazo ziko vizuri ni kadi za NHIF za Wabunge, lakini ilikuwa hai-cover vidonge tu vya uchungu. Kwa hiyo, mimi naiomba sana Serikali ikae iangalie vizuri sera, ipitie upya Sera ya Matibabu Bure kwa Wajawazito. Pia utakuta mama mjamzito ambaye anapata miscarriage anasafishwa kwa kati ya shilingi 300,000 mpaka 500,000. Kwa hiyo, nafikiri tunahitaji kuifafanua vizuri zaidi hii sera ili isituchonganishe na wananchi kipi ni bure, kipi tunatakiwa kukilipia.(Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kingine ambacho ninapenda kukizungumza kiko kwenye ukurasa wa 17, juu ya afya ya uzazi, mama na mtoto. Kiukweli Mheshimiwa Waziri Ummy Mwalimu na Naibu wake wanajitahidi kwa kiasi kikubwa sana kupambana kupunguza vifo vya mama na mtoto. Ila kuna kitu kimoja kinanisumbua siyo peke yangu, naona tuko watu wengi tu, pengine leo mngetusaidia kukitolea ufafanuzi ili kiweze kutusaidia.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwanamama anapokuwa mjamzito anapo-attend kliniki ni lazima, sijui kama ni lazima ama ni utaratibu wa kuwa anafanya ultra sound ili kuangalia maendeleo ya mtoto. Nikikumbuka mwenyewe aliyekuwa akinifanyia alikuwa anasema unaona mtoto wako huyu anaendelea vizuri, mapigo ya moyo, vidole vyake hivi vitano, hana mgongowazi, walikuwa wanasema hivyo. Ila kuna tatizo, wanashindwa kuangalia kama nitakosea kitaalamu mtanirekebisha, Mheshimiwa Dkt. Ummy na Mheshimiwa Dkt. Ndugulile, kuna kitu kinaitwa coding ama wanasema kitanzi, sijui kwa nini lile linashindwa kuangaliwa kipindi kile mama anapo-attend kliniki, kiasi kwamba…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha muda wa Mzungumzaji)

MHE. HAWA M. CHAKOMA:Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru, naunga mkono hoja.