Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi hii.

Kwanza kabisa nianze kwa kumshukuru Mungu na kumpongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na watendaji wote wa Wizara ya Afya, napenda kutoa shukrani kwa Serikali yetu ya Awamu ya Tano kwa mambo mazuri inayotufanyia Mkoa wa Morogoro. Imetupatia fedha kwa vituo vitano ambavyo ni Gairo, Mtimbira, Kidodi, Mkuyuni, Kibati na Rupiro. Kwa upande wa Mtimbira tumepata shilingi bilioni 500 kwa ujenzi pamoja na ukarabati na vituo vingine vilivyosalia tumepata shilingi bilioni 400 kwa kila kituo.

Mheshimiwa Naibu Spika, ombi langu kwa Mheshimiwa Waziri Ifakara Mji, Ifakara hawana Hospitali ya Wilaya na mara kwa mara wanatumia kibaoni Kituo cha Afya Kibaoni kama hospitali yao ya Wilaya. Maombi yalishaletwa ya kukipandisha kituo hiki kiwe Hospitali ya Wilaya. Kwa hiyo, naomba Mheshimiwa Waziri aweze kuona kuna haja ya kuipandisha hadhi na kuwa Hospitali ya Wilaya kwa sababu wanakihitaji hasa akina mama na watoto ambao mpaka sasa hivi majengo yapo, lakini kinachokosekana hakuna wodi ya watoto njiti ambao wanazaliwa kabla ya muda wao na wanachanganywa pamoja na watoto ambao wanaumwa, namna hii wanaweza wakapata maradhi kutokana na mchanganyiko huo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande mwingine naomba pia kwa upande wa hospitali ya Rufaa ya Mkoa ambayo mara nyingi tumekuwa tunaomba x-ray pamoja na chumba pekee cha upasuaji wa mifupa, nyote mnajua kuwa Mkoa wa Morogoro unapokea watu wengi ambao wanapa ajali, pia tunaomba gari la wagonjwa tuweze kuongezewa gari lingine kwa sababu Manispaa yetu ina kata 29 pamoja na Wilaya zingine ambazo hazina hospitali na zinatumia Hospitali hii ya Mkoa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuongezea hapo kuna Wilaya ambazo hazina hospitali kwa mfano Gairo, Kilombero nilivyosema pamoja na Morogoro Manispaa. Kwa hiyo, naomba sana kuwa tuweze kujengewa hospitali hizi kusudi kupunguza mrundikano wa wagonjwa kwenye Hospitali yetu ya Mkoa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Bima ya Afya ni mpango wa Serikali kuwa kila mmoja aweze kutumia bima ya afya. Kwa hiyo, mkakati uliowekwa na Serikali wa kuona kuwa kila mmoja aweze kutumia Bima ya Afya kuangaliwa kwa makini.

Mheshimiwa Naibu Spika, niongelee kuhusu suala la lishe, kwa ukweli kwenye upande wa nchi yetu ya Tanzania bado lishe inahitajika kwa wingi, bado tuna udumavu, bado tuna ukondevu na ninasema kuwa tuna malnutrition ambayo imepitiliza. Naomba hii mikakati ya ambayo wameiweka waweze kuitimiza na naomba kwa sababu suala la lishe ni mtambuka waweze kushirikiana pamoja na Wizara ya Kilimo kwa sababu unaweza ukatumia vyakula na ukapata vitamini pamoja na minerals.

Mheshimiwa Naibu Spika, upungufu wa wataalam wa Maendeleo ya Jamii. Ni ukweli usiopingika kuwa wataalam wa Maendeleo ya Jamii ndiyo wanaosukuma maendeleo kwenye Mikoa yetu, kwenye kata zetu na kwenye vijiji vyetu, uliangalie suala hili ili kusudi tuweze kuwa na wataalam wa Maendeleo ya Jamii kwenye kila kijiji na kwenye kila kata kusudi tuweze kusukuma maendeleo ambayo ndiyo yanatakiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuongelea uwezeshaji wa wanawake, kuna asilima tano ambayo pamoja na TAMISEMI naomba muweze kushirikiana na TAMISEMI ili kusudi hawa Maendeleo ya Jamii ndiyo wanasukuma maendeleo.

Mheshimiwa Naibu Spika, namalizia kwa kusema kuwa naunga mkono hoja na Mwenyezi Mungu akubariki kwa kunipatia nafasi hii na nawapenda sana. Ahsanteni sana.