Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Naibu Spika, nianze na pongezi kwa Waziri wetu Mheshimiwa Ummy Mwalimu, Naibu Waziri na watendaji wote wa Wizara kwa kazi nzuri sana ambayo wamekuwa wakiifanya kwa ajili ya Wizara hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, Hospitali ya Mkoa wa Iringa ina eneo finyu sana kutokana na muingiliano wa Gereza Kuu la Iringa na kusababisha Madaktari wetu Bingwa kuishi nje ya hospitali. Tunaomba kwa sababu Serikali ni moja, Gereza liondoke kupisha hospitali ili hata kuweza kujenga majengo mengine ya huduma.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wetu wa Iringa una upungufu wa wafanyakazi asilimia 60. Changamoto hii inasababisha matatizo makubwa sana mpaka katika Hospitali za Wilaya. Pia tuna changamoto Hospitali ya Mkoa haina Daktari Bingwa wa Watoto. Tunaomba Serikali iangalie kwa uzito mkubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu dawa MSD; niipongeze Serikali kwa upatikanaji wa dawa na nipongeze kwa kuleta moja kwa moja katika vituo vya afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu Bima ya Afya, tunaiomba Serikali suala la wazee, huduma ya wazee dawa ni ghali sana zipo nje ya mfumo wa bima yao, wanapata shida sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali iangalie watoto yatima walio katika vituo wanapata shida sana hawana bima ya afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ina mpango gani wa kuweka madawati katika vyuo vikuu. Nilipata bahati ya kukutana na Serikali za Wanafunzi wa Vyuo Vikuu. Wanafunzi wanachangia pesa lakini haziwasilishwi Bima ya Afya kwa wakati kwa ajili ya kupatiwa kadi za matibabu. Naomba Wizara ilichukue hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu tatizo la ugonjwa wa saratani; niipongeza Serikali kwa kuanza kutoa chanjo kwa mabinti zetu kuanzia miaka tisa hadi 15; hii ni hatua kubwa sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kupata ufafanuzi je, watoto wa kiume hawana haja ya chanjo hii? Huwa naona kuna kansa ya mabusha. Je, inawezekana chanjo hii wakapatiwa wanawake wenye umri wa zaidi ya miaka 15? Nimeona nchi nyingine wanapatiwa. Ni imani hata mkiweka malipo kwa ajili hiyo au bima ziweze kulipia chanjo hizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, lipo tatizo kubwa sana kwa wagonjwa wa saratani katika Mkoa wa Iringa kwenda Hospitali ya Ocean Road Dar es Salaam ni kwa nini Serikali isiweke centre za haya matibabu kikanda au matibabu yasogezwe Dodoma ili iwe rahisi kufikiwa na kupunguza gharama kwa sababu kina mama wanapata shida sana hata kimaisha wapokwenda Dar es Salaam kwa ajili ya matibabu hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu huduma ya matibabu ya moyo na figo; pongezi kubwa sana huduma hiyo imetupa moyo sana kuwa imeweza kupunguza hata gharama za matibabu ya nje ya nchi. Hongera sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.