Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Naibu Spika, upelekaji wa fedha za maendeleo katika Hospitali za Mikoa imekuwa wa kusua jambo ambalo linakwamisha shughuliza za utoaji wa huduma katika maeneo mbalimbali hapa nchini kwa kuwa mahitaji ya fedha za maendeleo ni mkubwa katika sekta na maeneo mbalimbali, hivyo basi naishauri Serikali kuliko kugawa fedha za miradi ya maendeleo kwa mtawanyiko wa nchi nzima bila kuonesha matokeo ya haraka na miradi kubaki viporo. Nashauri fedha za miradi ya maendeleo kila mwaka ipelekwe kikanda kwa kuangalia na kutanguliza maeneo yenye mahitaji makubwa zaidi. Hata hivyo ugawaji huu uendane na takwimu zinaonesha uhitaji upo kwa kiwango gani.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu upungufu wa watumishi katika sekta ya afya, sekta hii inakabiliana na upungufu wa asilimia 49 ya watumishi wa afya katika mwaka a fedha 2016/2017; changamoto hii imekuwa ya muda mrefu hasa maeneo ya vijijini jambo ambalo linapelekea wananchi kukosa huduma na hasa tukilinganisha idadi ya ongezeko la watu nchini. Naishauri Serikali kuhakikisha inaweka mkakati wa haraka wa kuhakikisha inakabiliana na changamoto hii kwani idadi ya watu nayo inaongezeka.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu chakula na lishe, tatizo la udumavu nchini ni kubwa kutokana na lishe duni kwa watoto na wajawazito, udumavu huu kwa watoto ambao ndiyo Taifa la kesho maana yake tutatengeneza Taifa la udumavu. Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na REPOA takribani watoto milioni 2.4 wana udumavu; takwimu hii ni kubwa na watoto hawa wengi ni wale walio katika kaya maskini za vijijini. Hivyo basi, Serikali ituambie ina mkakati gani wa kuiwezesha Taasisi ya Chakula na Lishe kifedha na kuweka mikakati ya haraka ya kukabiliana na hali hii ya lishe duni unaosababisha udumavu kwa watoto hapa chini.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu uzazi wa mpango, uwekezaji wa Serikali katika mpango wa uzazi ni jambo la muhimu sana kwani jambo hili limekuwa haliwekewi fedha za kutosha, umuhimu na uhusiano wa mpango wa uzazi na mkakati wa kupunguza vifo vya wanawake wajawazito; uzazi vina mahusiano ya karibu, hata hivyo kukiwepo na uzazi wa mpango ndivyo ambavyo tunaweza kupanga mipango bora ya maendeleo. Nashauri Serikali ihakikishe upatikanaji wa madawa, vifaa vya uzazi wa mpango katika maeneo yote ya utoaji wa huduma ya afya nchini. Serikali iongeze bajeti na kutoa fedha zilizoainishwa za fungu hili. Pia kuwa na huduma na vituo vya afya ya uzazi kwa vijana nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu pensheni kwa wazee; wazee wa nchi hii wamekuwa wakipewa matumaini ya kupatiwa pensheni bila mafanikio yoyote. Je Serikali ina mpango kati wa haraka wa kutoa pensheni kwa wazee nchini?

Mheshimiwa Naibu Spika, uwakilishi na usawa wa kijinsia, kwa mujibu wa takwimu za Employments and Earns Report ya mwaka 2015 nafasi za wanawake walioshika nyadhifa mbalimbali ni asilimia 15 tu ya idadi ya waajiri, wateuliwa na wachaguliwa wote nchini. Idadi hii ni ndogo sana. Hivyo basi Wizara iwajibike kuona ongezeko la usawa wa kijinsia katika nafasi mbalimbali unaongezeka zaidi, nawasilisha