Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Alfredina Apolinary Kahigi

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. ALFREDINA A. KAHIGI: Mheshimiwa Naibu Spika, nawashukuru sana kwa kazi mnazozifanya, tunaziona, kazana sana. Nashauri katika hospitali nyingi za vijijini hazina vitendea kazi vya kutosha, viongezwe; pili, wafanyakazi ni shida, unakuta wako wawili kazi zinawawia nyingi, wanachoka, hivyo basi lifanyie kazi suala hili waajiriwe wafanyakazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu dawa, baadhi ya dawa nyingine hatuzipati, hasa zile muhimu; fuatilia suala hili, tunaambiwa hazipo tununue katika maduka ya dawa ya watu binafsi.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho, wazee sehemu nyingine hawajapatiwa vyeti vya kutibiwa bure, wasaidie wazee; kama Kata ya Kanyangereko, Maruku, Nyakato na nyingine nyingi.