Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuchangia hoja iliyoko mezani leo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna changamoto nyingi sana kwenye Wizara ya Afya na kila mara imekuwa ikipangiwa bajeti ndogo sana kulinganisha na mahitaji. Sasa hivi kumekuwa na mkanganyiko mkubwa sana kati ya Wizara ya Afya na TAMISEMI. Kwa nini Serikali iliamua kuchanganya kazi za Wizara hizi mbili? Kwa mfano, inapofikia suala la majengo ni jukumu la TAMISEMI, halafu watumishi ni wa Wizara ya Afya. Ningependekeza masuala haya yote ya ajira na majengo yangetakiwa kuwa chini ya Wizara ya Afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine linahusu Jimbo moja kwa moja; wakati wa ziara ya Waziri Mkuu aliahidi kuleta gari la wagonjwa kwenye Zahanati ya Chiwale, napenda kufahamu ahadi kama imekufikia na utekelezaji wake utafanyika lini ukizingatia kwamba Jimbo la Ndanda lina kituo cha afya kimoja tu, kati ya Kata 16, hili lifanyike kwa wakati.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ni juu ya majengo; pamekuwa na sintofahamu kubwa sana juu ya aina ya majengo yanatotakiwa. Wananchi wanahitaji majengo ya kuweza kupatiwa huduma, lakini Serikali imetengeneza ramani ambazo kwa hali ya wananchi wetu ambao tumewataka weweze kukamilisha majengo haya mpaka hatua ya lenta ndipo Serikali itayapokea, lakini suala hili limekuwa gumu sana kutekelezwa kwa sababu ya uwezo mdogo wa wananchi pamoja na kukatishwa tamaa na hali ya kutokukamilishwa kwa majengo ambayo wananchi tayari wameshakamilisha majengo hayo. Pamoja na kuangalia miaka ya mbele, basi Serikali sasa ikubali angalau kukamilisha majengo ya zamani (maboma).