Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naanza kumpongeza Waziri kwa hotuba yake nzuri ya matumaini makubwa kwa Watanzania. Pia naipongeza Wizara ya Afya kwa juhudi zake za kuhakikisha kuwa Watanzania wanakuwa na afya bora wakiwemo wananchi wa Nyang’hwale.

Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri wangu kama Mbunge kwa Wizara hii ni kuhakikisha pesa zinakwenda kwa wakati katika hospitali, vituo vya afya na zahanati zetu. Wizara imepanga kutoa chanjo kwa watoto wa kike ya saratani ya shingo ya kizazi. Kikubwa elimu itolewe huko vijijini ili wananchi waondokane na hofu ya chanjo hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, ombi langu; Kituo cha Afya Kharumwa kina upungufu wa wataalam wa afya, vifaatiba, X-ray na kadhalika, pia dawa hazitoshi, wodi hazitoshi na zilizopo ni ndogo sana zina vitanda vinane kwa wanaume na wodi ya mama na mtoto ina vitanda 20 tu.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Halmashauri ya Nyang’hwale vitambulisho vya wazee bado hawajapewa, kwa hiyo hawapati haki yao ya matibabu bure. Je, ni lini watapewa vitambulisho vyao?

Mheshimiwa Naibu Spika, hatua kali zichukuliwe kwa watu wanaonajisi na kubaka watoto wadogo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nawapongeza sana Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri kwa kutoa gari la wagonjwa Kituo cha Afya Kharumwa. Wananchi wanawapongeza sana na wanaomba kwa Mungu muendelee na moyo huo.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumuuliza Mheshimiwa Waziri ni lini Kituo cha Afya Kharumwa kitapandishwa na kuwa Hospitali ya Wilaya? Hadi sasa inaitwa Hospitali ya Nyang’hwale lakini haijapata hati hadi leo.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naunga mkono hoja bajeti hii ya Wizara.