Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Ruth Hiyob Mollel

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. RUTH H. MOLLEL: Mheshimiwa Naibu Spika, Dar es Salaam ina wakazi takribani milioni tano na Wizara ilikuwa na azma ya kuimarisha Hospitali za Temeke, Ilala na Mwananyamala ili kusogeza huduma za kibingwa kwa jamii na kupunguza msongamano kwenye Hospiatli ya Rufaa ya Muhimbili. Lengo hilo la kuimarisha hospitali kwenye Wilaya hizo halijafanikiwa na hivyo msongamano wa wagonjwa umeendelea kuwa kero. Naishauri Serikali kuimarisha hospitali hizo ili kusogeza huduma kwa jamii na kupunguza msongamano wa wagonjwa kwenye Hospitali ya Rufaa ya Muhimbili.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na juhudi kubwa ya kupeleka wataalam wa fani mbalimbali kwenye vituo vya afya na dispensaries, bado upungufu ni mkubwa na umeongezeka zaidi baada ya kufukuza watumishi wenye vyeti fake, wengi wao wakiwa wataalam wa afya. Ni muhimu sasa kwa Serikali kupeleka wataalam wa kutosha ili kupunguza ratio ya wagonjwa kwa wataalam wa afya. Kama WHO standard ni daktari 1:10,000 lakini kwa Tanzania ni daktari 1:25,000, uwiano huu ni mkubwa sana na inafanya madaktari kulipua kazi bila ya kutumia muda wa kutosha kumsikiliza mgonjwa, kumpa ushauri nasaha na mwishowe tiba.

Mheshimiwa Naibu Spika, naishauri Serikali itekeleze mkakati maalum wa kutoa mafunzo kwa watumishi wa afya na kuhakikisha wanapunguza kazi kwenye maeneo mbalimbali. Serikali ianzishe mkakati wa kutoa motisha kwa watumishi wanaopangwa maeneo magumu yasiyokuwa na miundombinu rafiki.