Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Goodluck Asaph Mlinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Naibu Spika, hali mbaya ya Hospitali ya Wilaya ya Ulanga, majengo ni chakavu na machache. Wataalam (wahudumu wa afya) wapo wachache na wasio na sifa, gari la wagonjwa lipo moja ambalo nililikarabati mimi Mbunge na mahitaji ni makubwa sana; upatikanaji wa dawa bado hauridhishi kutokana na kuchelewa usambazaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, NHIF bado kumekuwa na ugumu kwa baadhi ya mashirika ya umma kujiunga kama takwa la kisheria. Mfano BOT mpaka sasa hawajajiunga.