Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Naibu Spika, bajeti inayopitishwa na Bunge ipelekwe kwenye maeneo husika na muda muafaka ili kuondoa changamoto wanazokutana nazo wananchi katika maeneo mbalimbali nchini hasa maeneo ya vijijini.

Mheshimiwa Naibu Spika, kulingana na ongezeko kubwa la watoto wa mtaani Serikali iongeze maeneo ambayo watu watapewa msaada pale inapobidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, mapungufu ya Maafisa Maendeleo ya Jamii katika Halmashauri zetu ni jambo ambalo limekuwa changamoto katika huduma mbalimbali za kijamii kulingana na uchache wa watumishi katika maeneo mbalimbali nchini. Pia upungufu wa Madaktari Bingwa katika Hospitali ya Rufaa katika Mkoa wa Rukwa na hospitali hii inazidiwa na wagonjwa kwa kuwa hatuna Hospitali ya Wilaya hata moja katika Mkoa wa Rukwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu dirisha maalum kwa ajili ya wazee; hospitali nyingi hazina dirisha maalum kwa ajili ya wazee na maeneo ambayo wamejitahidi kuweka dirisha kwa ajili ya wazee hakuna huduma. Nashauri Serikali kufatilia suala hili kwani wazee wetu wanapata taabu sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu afya ya akili; Serikali iwekeze kwenye utafiti kujua nini kinasababisha suala hili kuendelea kwani idadi ya waathirika wa akili inazidi kuongezeka.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni vyema Serikali ikawekeza kwenye lishe kwani tusipowekeza kwenye lishe tunakwenda kuzalisha watoto wenye udumavu wa akili.