Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Abdallah Majurah Bulembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. ABADALLAH M. BULEMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwanza kabisa kwa sababu dakika tano ni chache, nichukue nafasi hii kumpongeza Waziri Mbarawa na wasaidizi wake, Katibu Mkuu, wasaidizi wake wengi wa taasisi mbalimbali, kazi mnayofanya inapendeza, tunawaona kila siku mnavyochapakazi, hongereni sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nijikite kwanza kwenye eneo la Mamlaka ya Viwanja vya Ndege. Kiwanja cha Ndege cha Musoma nimeona mmeweka pesa fulani hapa, lakini shughuli yake haitakuwa nzuri, lipeni wale watu fidia basi; kwa sababu tusipate hela halafu fidia ikawa shida. Muanze fidia twende kwenye uwanja, lakini tukianza uwanja watu watakwenda Mahakamani itaonekana kero.

Mheshimiwa Mwenyekiti, namba mbili, Kiwanja cha Ndege cha Bukoba; mmefuta ile Mkajunguti ambayo ilikuwepo kuanzia karibu miaka 43, tumesema tunakwenda pale Bukoba, basi tulipeni fidia tupanue uwanja ule, kwa sababu ndege chache zinatatua pale kama uwanja huo hautaweza kupanuliwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, uwanja mwingine ni Sumbawanga pale, mimi naongea Kitaifa kidogo. Pale Sumbawanga nao walipeni fidia uwanja uwepo. Sasa kwa sabbau eneo hili sehemu fulani imekwenda TANROADS ni vizuri sana mkasimamia zaidi angalau viwanja na ndege Bombadier zinakuja nyingi tunawapongeza ili ndege zifike kila mahali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nipongeze standard gauge, kwa maana ya TRC. Hawa watu wanafanyakazi kubwa sana ambayo ilikuwa haijafanyika siku zote, na ni kitu cha historia. Lakini naomba wale wanaokwamisha kuzuia kubomoa Serikali ifanye kazi yake kwa sababu Serikali inatakiwa kutenda. Huwezi kubomoa kuanzia Dar es Salaam ukifika pale katikati ya Tabora mtu anakataa, standard gauge itafikaje? Tuwape ushirikiano na Wizara yako Mheshimiwa Mbarawa endeleeni kufanya ukali, haki ipatikane sisi tunataka maendeleo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna shida kuhusiana na minara ya simu. Sisi tunatoka kwenye mikoa ya mbali kule. Ukianda pale Musoma, Sirari ukisogea kidogo inainga Safaricom, ukienda maeneo ya pale Bukoba karibu na Mutukura inakuja tena inaonekana unaanza kutumia roaming, wale wananchi mnawatesa, ni Watanzania, lakini nguvu ya upande wa pili inakuwa kubwa zaidi katika kutumia mawasiliano, kule tatizo lake naomba mtusaidie. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nirudi kwenye TTCL, naomba niwapongeze Mwenyekiti Nundu na kijana Kindamba, kazi yenu ni kubwa mnayoifanya. Leo nilishawishi Bunge hili, kwa nini Wabunge mnakwenda Vodacom, Tigo hamtaki TTCL? Ndiyo yetu hii, ndiyo mali yetu. Mimi naomba tutumie hoja yangu kwamba kila mmoja akitoka nje ajiunge na TTCL, ni muda mfupi ujao miaka miwili TTCL itakuwa imepanda kuliko kampuni nyingine. Lakini unaweza kukuta hata ninyi Mawaziri TTCL hampo. Ninyi ni Mawaziri mnatumia pesa ya Serikali, TTCL hamjajiunga. Kwa kupitia hoja hii Waziri Mkuu, naomba Mheshimiwa Waziri Mkuu uwaulize Mawaziri wako wangapi wako ndani ya TTCL, ndiyo kwa sababu wanatumia hela yetu ya kodi lakini hawajiungi na TTCL. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni kuhusu Bandari ya Dar es Salaam; nichukue fursa hii kuupongeza utawala ulioko Dar es Salaam, mambo yanatoka pale, mizigo inaondoka haraka. Tunaomba nguvu hiyo isirudi nyuma kwa sababu wako wachache wanaokwamisha kwamisha juhudi zile. Wachukulieni hatua sisi tuendelee kupiga maendeleo katika nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho ni kuhusu TANROADS. Hivi TANROADS Mheshimiwa Mbarawa, TARURA mmewapa asilimia 30 si mkae mapema muongezee hata wapate 40, barabara ni nyingi za vijijini kuliko hizi barabara kuu? Kwa nini mnajipendelea? Maendeleo ni yetu wote, kwa sababu TARURA wana safari ndefu zaidi na ndiyo wanaanza.

Nasikia kwenye bajeti ya juzi nao viwango vya mishahara hamtaki kuwapa, hapana, tuwe fair, TANROADS wanaopata…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. ABADALLAH M. BULEMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.