Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Godfrey William Mgimwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. GODFREY W. MGIMWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuchangia. Awali ya yote, nimshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kunipa nafasi hii, lakini vilevile nichukue nafasi hii kumshukuru sana Rais wetu mpendwa, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa kazi nzuri ambayo anaendelea kuifanya kwa Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nichukue nafasi hii kushukuru Wizara, Waziri husika, Mheshimiwa Profesa Mbarawa na wasaidizi wake wote. Kazi tunaiona na tunaendelea kuwa-support, tupo nyuma yenu, endeleeni kufanya kazi na tunaamini Tanzania itaendelea kubadilika kwa muda tunaotarajia kuweza kufika huko mbele. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze tu kwa kusema kwamba Wizara ya Ujenzi ni muhimu sana katika Taifa letu lakini hatuwezi tukasonga mbele kama tutakuwa hatuangalii au tuka-review bajeti zetu ambazo tunazipitisha mwaka baada ya mwaka. Kuna mambo mengi ambayo yameelezwa bajeti iliyopita mwaka 2017/2018 na 2018/2019 kuna baadhi ya mambo ambayo nimeangalia kwenye hotuba na nimeona yanakwenda vizuri lakini bila kuangalia tulichokifanya mwaka jana na mwaka juzi tunaweza tusiweze kufika tunakoenda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala kubwa ambalo tunaliangalia la TARURA na TANROARDS ambako tunakuta asilimia 30 kwa asilimia 70 ya maendeleo. Sasa tuangalie uwezekano kwa sababu TARURA tuna barabara nyingi, zaidi ya 100,000 ambazo tunatarajia kuzitengeneza lakini asilimia ambayo imetengwa ni ndogo sana. TARURA inaangalia vijijini ambako ndiko kwenye watu wengi na ndiko kwenye tija. Napenda kuishauri Serikali namna gani ambavyo tunaweza tuka-balance sasa at least tupeleke kwenye 40% kwa 60%.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba viwanja vya ndege vimeendelea kujengwa katika maeneo mbalimbali lakini niseme mahsusi kwa Kiwanja cha Nduli ambacho kipo Iringa. Kiwanja hiki cha ndege ni cha muhimu sana. Upande wa Nyanda za Juu Kusini ndiyo tuna Kiwanja cha Songwe ambacho Serikali imeshatenga fedha lakini naamini kabisa Kiwanja cha Nduli ambacho kipo Iringa kitakuwa ni sehemu ya ukuaji wa uchumi katika Nyanda za Juu Kusini. (Makofi)

Nimshukuru sana Makamu wa Rais alikuja Jimboni na alikuja Mkoani Iringa na akaangalia maendeleo ya mkoa.

Kupitia Benki ya Dunia tumepata ufadhili wa kujenga ile barabara ya kutoka Iringa Mjini kuelekea Ruaha National Park kwa kiwango cha lami. Hiyo peke yake ni maendeleo ya makubwa sana kwa Taifa letu na watu wa Iringa tunajivunia sana kwa sababu tunaamini sasa tutaenda kupata uchumi ambao tunautarajia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba maendeleo bila barabara au bila kuhakikisha kwamba masuala mazima ya usafiri wa anga yanakaa vizuri bado tunaweza tukawa nyuma tukijilinganisha na nchi zingine za Afrika Mashariki. Niseme tu kwamba Tanzania tumejipanga vizuri na naamini kabisa kwa Awamu hii ya Tano tunaenda vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niishauri Serikali katika eneo moja, kuna mikataba mbalimbali ya usafiri wa anga ambayo Serikali inaingia inaitwa Bilateral Air Service Agreement, Tanzania bado tuko nyuma kidogo, tuingie mikataba mingi na mashirika mbalimbali ya kimataifa ili ndege mbalimbali ziendelee kufika Tanzania na sisi tuweze kurusha ndege zetu katika viwanja mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kenya wenzetu wameshasogea sana, Uganda nao wanakwenda sisi Tanzania mpaka mwaka 2017 tulikuwa tumeingia mikataba mingine mipya 10, hiyo haitoshi. Napenda kushauri Serikali kwamba bila kuingia mikataba mikubwa ya namna hii tunaweza tukabaki nyuma. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine kubwa ni la PPP. Naamini kabisa maendeleo yetu Watanzania bila PPP tunaweza tukawa nyuma, tunaweza tusifanikiwe. Ni lazima tufanye utaratibu wa kuji-engage sisi wenyewe katika miradi ya PPP. Wenzetu wa Rwanda wamejenga uwanja wa Busegera ambao ni asilimia 25 kwa asilimia 75, utakuwa ni uwanja mmoja mzuri sana katika ukanda wa Afrika Mashariki. Naamini kwa sababu wameamua kufanya hivyo sio lazima watumie fedha zao zote. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi bado tuko nyuma kimaendeleo. Afrika tunahitaji tuweze kujilinganisha na nchi zingine lakini tutafikaje huko tunakotaka kwenda kama tutakuwa tunatumia nguvu zetu nyingi bila kushiriki katika uchumi unaostahili…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)