Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Joyce John Mukya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. JOYCE J. MUKYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia katika Wizara hii ya Ujenzi, Uchukuzi, Mawasiliano kwenye bajeti ya mwaka 2018/2019. Nitakuwa na hoja tatu kama muda utatosha, kwa sababu muda ni mchache, naomba nianze moja kwa moja kwenye hoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kuongelea karakana ya kuhifadhi na kutengeneza ndege ambayo iko katika Uwanja wa Ndege Kilimanjaro. Karakana hii ilinyang’anywa kwa mwekezaji wa VIA Aviation ambaye alikuwa anaitwa Susan Mashibe Februari, 2016 ambaye aliambiwa alikuwa anatoa ushuru kidogo. Alikuwa analipa dola 3,000 kwa mwezi na Serikali inasema alikuwa anapata hela nyingi sana lakini alikuwa anatoa ushuru kidogo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niiulize Serikali, mpaka wanakubaliana awe analipa dola 3,000 alijipangia mwenyewe au waliandikishiana mikataba na yule mwekezaji ambaye ni VIA Aviation alipe dola hizo kwa mwezi. Kazi hii kaifanya kwa muda wa miaka 10 na yeye kwa sababu alikuwa anajua anatakiwa alipe dola 3,000 kwa mwezi ikabidi awe anatengeneza ndege nyingine ambazo siyo za ATCL lakini kwenye mkataba ilikuwa atengeneze ndege za ATCL.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, tunajua kwamba ndege za ATCL zimeanza kazi hivi karibuni. Ndege zilikuwa hazifanyi kazi lakini mwekezaji huyu alikuwa anatakiwa alipe dola 3,000 kwa mwezi, je, angefanyaje ili aweze kulipa dola hizo kwa mwezi kwa Serikali ya Chama cha Mapinduzi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwekezaji yule sasa hivi hana kazi lakini pia Serikali ya Chama cha Mapinduzi imefungia vile vipuri na ndege za ATCL zinatengenezwa nje ya nchi kwa gharama kubwa sana. Vipuri vimefungiwa katika Uwanja wa Ndege wa Kilimanjaro na ndege hazitengenezwi tena katika uwanja huo bali zinapelekwa nje.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali, matengenezo madogo madogo ya ndege yafanyike pale katika karakana ya Kilimanjaro yaani Uwanja wa KIA kwa sababu kwa kupeleka ndege nje wanapoteza fedha nyingi sana za Tanzania na wakati pale KIA kuna karakana ya kutengeneza na kuhifadhi ndege za ATCL. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naelekea TBA, wazee wa expansion joint. TBA ambao wanahusika zaidi kutafuta viwanja kwa ajili ya Serikali, kujenga nyumba kwa ajili ya watumishi wa umma mbalimbali, wamekuwa wanajenga nyumba hizi lakini hawajui kuzigharamia. Mfano mzuri ni hapa Dodoma katika eneo la Site One, Sengia (Area D), wamejenga nyumba pale kuanzia mwaka 1994 mpaka leo ni miaka 24, hawajawahi kurudia hata kupaka rangi ya ukuta wa nje achilia mbali kukarabati nyumba moja moja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukienda pale unatafuta njia ya kuingilia kwenye compound, huoni njia kumejaa majani kila mahali. Mnakaa majumbani mwenu kwenye mikoa yenu lakini mkifika Dodoma kwa ajili ya Kamati na Bunge majani yamejaa kila mahali, eneo ni chafu, hakuna sehemu ya kupita, mkikaa baada ya siku mbili ndiyo hao TBA mnaona wanaanza kuja kufanya usafi na kufagia, walikuwa wapi wasifanye usafi wakati nyie hampo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, mbali na hiyo, nyumba zile ambazo zina vyumba viwili wanalipa Sh.150,000 kwa mwezi, vyumba vitatu ni Sh.250,000 kwa mwezi, hela hizo zinakwenda wapi? Miaka 24 hata kama ni kurudisha gharama wamesharudisha gharama, kwa nini wanajenga majengo lakini hawayafanyii maintenance? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu kingine, hawa hawa TBA wanakwambia wanafanyia marekebisho nyumba za viongozi tu lakini pale Sengia, Site One wanakaa viongozi ambao ni Wabunge lakini nyumba zao hazifanyiwi matengenezo, zinafanyiwa matengenezo nyumba za Makatibu Wakuu ambao wanakuja kuhamia Dodoma kwa ajili ya Wizara zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, unaambiwa wewe ambaye unataka kufanya matengenezo kwenye nyumba yako, baada ya kufanya matengenezo aidha uweke tiles au ubadilishe choo mkae na TBA tena chini mkubaliane gharama mpya ya kodi ya nyumba wakati mpangaji ametengeneza nyumba peke yake na kwa gharama zake. Kama TBA wanataka kweli hela kwa nini wasifanye matengenezo wao wenyewe na baada ya hapo wakaongeza hizo gharama za kodi za kila mwezi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hiyo siyo sawa kabisa naomba sana hawa TBA wachukue jukumu lao la kujenga nyumba zao, wazifanyie ukarabati, zile nyumba zimechoka na kwao viongozi siyo Wabunge ni Makatibu Wakuu wa Wizara mbalimbali. Naomba sana hawa TBA wazifanyie ukarabati zile nyumba kwani zimechoka.