Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Pascal Yohana Haonga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbozi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kukumbushia ahadi ya Waziri Mkuu Mheshimiwa Kassim Majaliwa alipokuja Mkoa wa Songwe mwaka 2017 ambapo aliahidi mbele ya Wanambozi kwamba bararaba ya kutoka Mlowo - Kamsamba - Kilyamatundu (Rukwa) itatengenezwa kwa kiwango cha lami. Ukisoma ukurasa wa 222 wa hotuba ya Waziri barabara ya Mlowo – Kamsamba yenye urefu wa kilometa 130 imetengewa shilingi milioni 120 tu, je, fedha hizi zitatengeneza lami ya kilometa 200 kweli?

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa heshima na taadhima, naiomba Serikali itekeleze ahadi yake ya kutengeneza barabara hii kwa kiwango cha lami kama ilivyoahidi kwa wananchi. Barabara hii inaunganisha Mkoa wa Songwe na Rukwa na ni suala la kisera kuunganisha barabara zote ambazo zinaunganisha mikoa.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia barabara inayounganisha Wilaya ya Mbozi na Songwe kupitia Kata ya Magamba (Songwe) na Kata ya Mgamba (Mbozi) haijatengenezwa hata kwa kiwango cha changarawe jambo ambalo linawanyima fursa wananchi wa Wilaya ya Songwe kufika Makao Makuu ya Mkoa wa Songwe ambayo yapo Wilaya ya Mbozi. Wananchi wa Wilaya ya Songwe hulazimika kupitia Mbalizi, Mkoa wa Mbeya ili kufika Makao Makuu ya Mkoa. Naishauri Serikali itengeneze barabara hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.