Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja hii. Hata hivyo nina ushauri kwa Wizara kwa mambo yafuatayo:-

(i) Barabara ya Kidahwe – Kasulu (kilometa 63); barabara hii imeanza yapata sasa miaka 13 haijakamilika na ujenzi wake ni takribani asilimia 30 tu. Tatizo kubwa ni kwa sababu barabara hii pamoja na kipande cha Kabingo/ Nyakanazi (kilometa 50) hazipewi kipaumbele kabisa. Tafadhali namwomba Waziri a-fast track process ya kujenga barabara hizi kama sehemu ya barabara kubwa ya Kidahwe – Nyakanazi. Sisi wananchi wa Kigoma sasa tumechoka kusubiri barabara hii. Kwa maoni yangu juhudi zinazoendelea ni njema lakini muda ni jambo la msingi sana. Haiwezekani tusubiri zaidi ya miaka 26 barabara hii.

(ii) Barabara za Lake Tanganyika chini ya Lake Tanganyika Transport Programme (LTTP/FS&DD), hizi ni barabara zipi na zina urefu gani?

(iii) Barabara ya Kasulu – Manyovu, chini ya mpango wa barabara za Afrika ya Mashariki inaanza kujengwa lini? Timeline yake ikoje? Tusubiri tena miaka mingapi?

(iv) Ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha Standard Gauge; juhudi zinazofanyika kujenga reli hii ni za msingi sana, Dar es Salaam - Morogoro na Morogoro - Makutupora kazi inaendelea vyema. Ajabu ni shilingi bilioni 100 kutengwa kwa ajili ya Isaka – Rusumo - Kigali. Mantiki ya kibiashara na kiuchumi ya kuanza kujenga kipande hiki ni nini hasa? Je, ni kuisaidia nchi ya Rwanda kupata reli au ni kuifanya Kigali iwe business hub ya nchi za Maziwa Makubwa?

Mheshimiwa Naibu Spika, binafsi siungi mkono kabisa ujenzi wa kipande hiki kwa sasa kabla ya kujenga kipande cha Dodoma - Tabora. Pesa hiyo shilingi bilioni 100 ihamishwe na ipangwe kujenga kipande cha Dodoma - Tabora. We have to be strategic and forward looking. Tukifanya makosa shida na adhabu yake ni kubwa sana. Reli ni uchumi mpana.

(v) Mawasiliano vijijini na mijini; minara ya simu sehemu mbalimbali za nchi yetu ipo vizuri. Hata hivyo, baadhi ya maeneo ya Kata ya Muhunga, Kijiji cha Marumba mawasiliano ni taabu sana. Ili upate network yakubidi upande mti au usimame juu ya kichuguu. Aidha, katika Kijiji cha Karunga, Kata ya Heru Juu mtandao unasumbua sana.

KIJIJI KATA JIMBO WILAYA
Karunga Heru Juu Kasulu Mjini Kasulu
Marumba Muhunga Kasulu Mji ni Kasulu
Mwanga Mganza Kasulu Mji ni Kasulu

Tafadhali sana wenzetu wa Mawasiliano kwa Wote wafanye juhudi ili kuondokana na usumbufu huu kwa wananchi wetu.