Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Naibu Spika, naipongeza sana Wizara hii kwa kazi nzuri ya barabara iliyofanyika Singida Mjini. Naipongeza TANROADS kwa usimamizi mzuri wa barabara hizi hususani Singida Mjini.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimetazama bajeti ya Wizara hii sijaona utekelezaji ama mkakati wa utekelezaji wa ahadi ya bypass kilometa 84 kwa kuanzia tungeanza na kilometa 46 hali itakayotusaidia kupunguza msongamano wa magari makubwa kupita katikati ya mji. Naomba Serikali kuzingatia maombi haya.