Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Selemani Said Bungara

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Kilwa Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. SELEMANI S. BUNGARA: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu. Naomba kujua ahadi ya Rais ya barabara ya Kwa Mkocho – Hospitali ya Wilaya ya Kilwa na ahadi ya Rais ya kujengwa kiwango cha lami kilometa nane katika Mji Mdogo wa Kilwa Masoko.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujua malipo ya wananchi waliothaminiwa katika maeneo ya mradi wa Uwanja wa Ndege wa Kilwa Masoko. Naomba kwa heshima na taadhima wananchi hao walipwe.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka kujua Bandari ya Kilwa Masoko upo mpango upi wa kuiendeleza kwa kuwa ni bandari muhimu hasa kwa kuwa upo mpango wa kujengwa kiwanda kikubwa cha mbolea.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mji Mdogo wa kihistoria wa Kivinje miundombinu ya barabara ni mibaya. Mifereji, barabara na madaraja ya Mji Mdogo wa Kivinje, hakuna bajeti wanayopanga. Naomba Mji Mdogo wa Kivinje utengewe fedha za kujenga miundombinu ya barabara, mifereji na madaraja.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Mji wa Masoko tuna kiwanja cha ndege. Kutokana na Mji wa Kilwa Masoko na Kilwa kwa ujumla kukua ni muhimu kuimarishwa na kupanuliwa kwa uwanja huo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa heshima na taadhima, naomba Mheshimiwa Waziri azingatie maombi na ushauri wangu. Natanguliza shukrani, ahsante.