Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Naibu Spika, katika Mkoa wa Rukwa tunategemea Uwanja wa Sumbawanga Mjini kwa ajili ya usafiri wa anga ambao umefanyiwa uthamini lakini mpaka sasa hatujui kinachoendelea.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kiwanja cha Ndege cha Nkasi, Makao Makuu ya Wilaya ambayo yako Namanyere, tunaomba maboresho makubwa ili wananchi wake wanufaike.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la barabara ya Ntendo – Muze ni barabara muhimu sana kwani ikiboreshwa itawasaidia wananchi wa maeneo hayo wanaojishughulisha na biashara ndogo ndogo na kuwainua kiuchumi.

Mheshimiwa Naibu Spika, bomoa bomoa inawaacha wananchi wengi wanaathirika na sheria iliyopo ambayo inazungumzia mita 15 kwa mjini na mita 30 kwa vijijini. Tunaomba sheria hii iletwe ndani ya Bunge ifanyiwe marekebisho.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kata ya Kala haina mawasiliano kabisa pamoja na Kata ya Ninde bado mawasiliano yake siyo ya uhakika. Naomba Serikali ipeleke mawasiliano.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba TARURA wapewe fedha za kutosha ili waweze kufanya kazi zao kwa haraka na uhakika. Pesa zikipelekwa kwa muda muafaka itaepusha madhara ambayo yanajitokeza kwa wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara zinazounganisha mikoa zipewe kipaumbele ili kuleta baraka kwa wananchi kwa kuwainua kiuchumi, lakini kuepusha vifo vya wanawake na watoto.

Mheshimiwa Naibu Spika, meli ya Ziwa Tanganyika (MV Liemba) imekuwa ya muda mrefu ambayo hata ikifanyiwa matengenezo bado imechakaa. Naishauri Serikali kutafuta meli nyingine mpya ambayo itawasaidia Watanzania.