Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Andrew John Chenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. ANDREW J. CHENGE: Mheshimiwa Naibu Spika, natoa hongera for a good and comprehensive speech. Nina issue mbili.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mara ya kwanza katika historia ya Wizara hii, barabara ya Kolandoto – Lalago – Mwanhuzi – Mataka - Mang’ola - Old Junction haikutajwa katika body ya hotuba ya Mheshimiwa Waziri, imefichwa kwenye kiambatisho Na. 3. Nilitegemea vipande vya barabara hiyo ambavyo FS/DD ulikamilika zamani (Kolandoto hadi Mwanhuzi na Sibiti) vingeanza kutengewa fedha kwa ajili ya ujenzi. Ikumbukwe kuwa barabara hii imekuwepo kwenye mipango ya Serikali tangu mwanzoni mwa miaka ya 1990.

Mheshimiwa Naibu Spika, Makao Makuu ya Mkoa wa Simiyu - Bariadi haujaunganishwa kwa barabara ya lami kati yake na Mkoa wa Singida na Arusha. Sehemu ya kutoka Kolandoto – Mwanhuzi - Sibiti) FS/DD umekamilika. Ni vema sasa FS/DD ikaanza katika ya Ng’oboka –Mwandoya – Kisesa - Bariadi. Sehemu ya kipande hiki kipo katika Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2015 - 2020. Naomba kuwasilisha.