Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Dr. Haji Hussein Mponda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. DKT. HADJI H. MPONDA: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja. Nampongeza Mheshimiwa Waziri Profesa Mbarawa, Naibu Mawaziri wote na timu nzima ya utendaji wa Wizara kwa kazi nzuri wanayotekeleza katika kutimiza majukumu ya Wizara. Pongezi pia kwa TANROADS Manager wa Morogoro, Engineer Doroth Mtenga na timu yake kutekeleza majukumu yao katika mazingira magumu na ufinyu wa bajeti.

Mheshimiwa Naibu Spika, sera ya barabara ni kuunganisha barabara za kuunganisha Mikoa ziwe za lami. Ni lini barabara ya Ifakara – Lupilo – Malinyi - Kilosa Mpepo – Londo – Lumecha – Songea itaanza ujenzi wa lami? Barabara hii ni ahadi ya Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli na muda umebakia kidogo na utekelezaji wa ahadi ya Rais mwaka 2020.

Mheshimiwa Naibu Spika, Sera ya Barabara inaelekeza kujenga barabara za Makao Makuu kwa kiwango cha lami. Wilaya ya Malinyi tunapendekeza/kuomba kuanza ujenzi wa barabara ya lami kwa kilomita mbili katika Mji wa malinyi. Ombi letu halitekelezwi. Tunaomba kauli ya Waziri, atueleze ni lini ataanza kutenga bajeti ya kuanza kujenga barabara ya lami katika Mji wa Malinyi (Makao Makuu ya Wilaya)?

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.