Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Suzana Chogisasi Mgonukulima

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. SUZANA C. MGONUKULIMA: Mheshimiwa Naibu Spika, matatizo ya barabara Mkoani Iringa yamekithiri. Ninaomba Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano ilichukue jambo hili kwa umakini ukizingatia mkoa huu unachangia pato la Taifa kwa kiasi kikubwa sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, natoa ushauri kwa Waziri wakati wa matengenezo ya barabara hasa kwa kutumia kifusi, kitumike kifusi ambacho hakina mawe yenye ncha kali, kama kifusi kilichowekwa barabara kutoka Tagamenda - Kitayawa - Ndiwili pamoja na Kidabaga; kifusi hicho kinasababisha uharibifu wa tairi za magari.

Mheshimiwa Naibu Spika, natoa ushauri kwa Waziri wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano wakati wa ujenzi wa barabara za lami kushirikisha Serikali za Vijiji kuwa walinzi wa alama za barabarani kwa kuwa wakati wa ziara iliyofanywa na Kamati ya Miundombinu tumekuta baadhi ya wananchi wanazitoa alama hizo na kusababisha ajali na upotevu wa hela za Serikali.