Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Emmanuel Papian John

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. EMMANUEL P. JOHN: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naunga mkono hoja na jitihada za Serikali juu ya ujenzi wa barabara nyingi na kwa kiwango cha lami nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maombi yangu ni barabara ya NARCO (Hogoro) – Kibaya – Orkestmet Orjoro (Arusha); tunaomba ijengwe kwa sababu zifuatazo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, moja ni shortcut road ya kwenda Tanga; mbili, kwa sababu Kiteto ni eneo linalozalisha mahindi mengi sana kwa Kanda ya Kati na kulisha Jiji la Dar es Salaam; tatu, maombi yangu tunaomba hizi kilometa 91 NARCO – Kibaya zijengwe kiwango cha lami maana ni ahadi ya Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete alipofanya ziara mwaka 2014 alipokuwa ziara Wilaya ya Kongwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaomba Wizara iokoe mazao ya wakulima kuepusha gharama kubwa za usafirishaji wakati wa msimu.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaomba mawasiliano kwenye Kata za Raiseri, Loovera pamoja na Kata ya Sunya.

Mheshimiwa Naibu Spika, natanguliza shukrani zangu.