Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. GEORGE B. SIMBACHAWENE: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri na Naibu Mawaziri wake kwa kazi nzuri wanayoifanya.

Kuhusu barabara ya kutoka Mbande – Kongwa – Mpwapwa – Kibakwe hadi Chipogoro; barabara hii ni ahadi ya Mheshimiwa kujenga kwa kiwango cha lami. Hatua kadhaa zilianza kuchukuliwa, ikiwa ni pamoja na kuweka alama za “X”. Kinachotusikitisha ni kuona haipo katika mpango wowote katika orodha ya barabara mbalimbali ulizozitaja katika hotuba yako. Aidha sijaona fedha yoyote iliyotengwa kwa ajili ya shughuli yoyote ya maandalizi ya ujenzi. Hakika tumeshindwa kuelewa nini hatima yetu kwa majimbo ya Mpwapwa na Kibakwe, Mheshimiwa Waziri tunaomba msaada wako, naunga mkono hoja.