Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. ENG. RAMO M. MAKANI: Mheshimiwa Naibu Spika, hongera kwa timu nzima ya Wizara kwa kuendelea kuchapa kazi kwa ufanisi. Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Makatibu Wakuu, Wakuu wa Taasisi, wataalam na supporting staff wote.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu barabara na madaraja, nashukuru Serikali kupitia Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kuitengea fedha miradi ifuatayo katika Jimbo la Tunduru Kaskazini, Daraja la Fundimbanga, barabara ya Mkoa – Mjimwema – Ngapa – Tunduru - Nachingwea Border.Ninaomba utekelezaji wa miradi ifuatayo ambayo kimsingi ni ukamilishaji wa miradi ya barabara ya Nakapanga – Tunduru itengewe fedha ili ikamilike.

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya mchepuo (bypass) ya Mkapunda – Masonya, mzunguko wa barabara (roundabout) – crossroad location. Barabara hii ya Mjimwema –Ngapa – Tunduru/Nachingwea Border ni barabara ya mkoa na ni ya kiwango cha udongo (earth road), ni vema kuweka katika mpango kutenga fedha na kuijengea barabara hii kwa kuwa inaunganisha Mkoa wa Ruvuma na Mkoa wa Lindi. Pia kuna daraja la Mto Lumesule katika barabara hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu uwanja wa ndege wa Tunduru, nafahamu kuwa vipaumbele kwa sasa vimewekwa katika viwanja vikubwa, viwanja vya Mikoa na vya kimkakati. Lakini ni ushauri wangu kwamba vigezo/ vipaumbele vijumuishe maeneo ya mpakani, maeneo yaliyoko mbali sana na viwanja vya ndege vinapotumika; kwa Tunduru kilometa 410 na kilometa 262 kutoka pande zote mbili, viwanja vya ndege vilivyokuwepo vikafungwa maeneo mapya yaliyofunguka na yenye potentials za kuchangia uchumi wa Taifa kiasi kikubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba uwanja wa Tunduru upewe kipaumbele.