Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Desderius John Mipata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Naibu Spika, nichangie kuhusu mawasiliano ya simu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kata ya Kala iliyoko mpakani kando kando mwa Ziwa Tanganyika ina vijiji vya King’ombe, Mtambo, Kilambo, Mpasa, Kapumpali, Tundu na Kala. Vijiji vyote hivi havina mawasiliano ya simu licha ya kuwa na zaidi ya watu 2,000 na ikumbukwe kuwa hawana barabara ya kuaminika. Mheshimiwa Waziri Mbarawa nimekuja kwako siyo chini ya mara sita au saba, nimeandika barua mbili na nimechangia hapa Bungeni zaidi ya mara 10 sijasikilizwa, je, ni kwa nini hasa?

Mheshimiwa Naibu Spika, binafsi sijaelewa kwa sababu pia hujawahi kunipa sababu ya msingi ya suala hili kutokuwezekana kwa muda wa miaka saba nikiwa hapa Bungeni. Naomba Wizara inisaidie kwani sieleweki kwa wananchi hawa. Vilevile kuna Vijiji vya Kasapa, Kata ya Sintali na Vijiji vya Kisambara na Msamba – Kata ya Ninde.

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Katongoro – Ninde; barabara ya Kitosi - Wampembe; barabara ya Nkana Kata zote zimefunga kutokana na mvua nyingi zinazonyesha huko Mkoani Rukwa na TARURA hawana fedha ya dharura. Naomba Serikali itoe fedha za dharura TARURA Nkasi vinginevyo wananchi hawapati huduma mbalimbali ikiwepo matibabu na bidhaa zingine za madukani.

Mheshimiwa Naibu Spika, niombe barabara ya lami toka Chala kuendelea kuunga Paramwe barabara ya lami imezunguka Makao Makuu ya Wilaya na kuacha barabara ya zamani ya kwenda Mpanda ambapo Vijiji vya Londokazi, Miombo, Mashete Mtenga na Mwai vimebaki na barabara ya vumbi na vijiji vya uzalishaji mkubwa wanaomba waunganishwe kwa barabara ya lami.

Mheshimiwa Naibu Spika, nitaunga mkono nikipata majibu ya mtandao Kata ya Kala, Nkasi Kusini.