Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Rukia Ahmed Kassim

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. RUKIA AHMED KASSIM: Mheshimiwa Naibu Spika, naanza kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri wa Mawasiliano pamoja na Naibu Mawaziri wake wawili, Mheshimiwa Makame Mnyaa Mbarawa na Naibu Mawaziri wake Mheshimiwa Engineer Atashasta Nditiye na Mheshimiwa Elias Kwandikwa kwa juhudi zao za kuijenga nchi yetu katika sekta hii ya ujenzi, uchukuzi na mawasiliano.

Mheshimiwa Naibu Spika, naanza na bandari; bandari ndiyo chanzo kikubwa cha mapato katika nchi yetu lakini bado ujenzi wa Gati Namba 13 hadi 14 katika Bandari ya Dar es Salaam unazorota. Toka mwaka 2010 tumeanza na wimbo wa ujenzi wa Gati hii Namba 13 hadi 14 mpaka leo haujaanza, jambo hili linazorotesha uchumi wa nchi. Naishauri Serikali itenge pesa kwa ajili ya ujenzi huu.

Mheshimiwa Naibu Spika, natoa pongezi za dhati kwa ununuzi wa ndege, tulikuwa hatuna ndege na ilikuwa ni aibu kubwa lakini leo nashukuru Serikali kwa ununuzi wa ndege. Naishauri Serikali kuwa na tahadhari ya kutosha katika kuhakikisha kuwa ATCL inajipanga kufanya kazi kwa faida. Kuna hujuma kubwa sana zinazofanywa na mawakala ambao wanatumiwa na mashirika binafsi.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo hili lilikuwa likifanywa na wakaua shirika hili. Ninaomba Serikali ifungue ofisi za kuuzia tiketi na siyo kutegemea mawakala. Unapokwenda kukata tiketi unaambiwa ndege imejaa lakini ukienda kuangalia airport ndege ni tupu haijajaa, mawakala wanakuambia ukate tiketi ya ndege nyingine kumbe siyo kweli wanataka ukate tiketi mashirika mengine.