Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Mahmoud Hassan Mgimwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. MAHMOUD H. MGIMWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nachukua fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri Profesa Mbarawa pamoja na Naibu Mawaziri wote wawili. Mchango wangu unajielekeza kwenye mambo yafuatayo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ni kuhusu barabara, hili ni eneo muhimu sana kwa uchumi katika jimbo langu la Mufindi Kaskazini na Wilaya Mufindi. Barabara ya kutoka Mtiri – Ifwagi – Mdaburo – Ihamu – Isipii – Mpanga TAZARA mpaka Mlimba inaunganisha mikoa miwili ya Iringa na Morogoro (Wilaya za Mufindi na Kilombero) lakini shida yake imekuwa kubwa sana kwani haipitiki kabisa na TARURA haina uwezo wa kuunga barabara hii. Ikumbukwe Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli aliahidi kuipandisha hadhi kuwa ya TANROADS. Mheshimiwa Waziri nimeshakuja kwako mara kadhaa lakini hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa kuinusuru barabara hii yenye uchumi mkubwa wa chai, kahawa, pareto, msitu wa mbao, maharage, mahindi na utalii ambao ungeongeza pato la Taifa letu.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni vyema sasa Mheshimiwa Waziri atupe mkakati wa kukabiliana na barabara hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya kutoka Kinyanambo A – Isalavani – Sadani – Madibira – Rujewa ambayo ipo kwenye Ilani ya Uchaguzi toka mwaka 2000 – 2005 - 2010 – 2015 – 2020, lakini hata kilometa moja tu haijajengwa. Ni vyema Mheshimiwa Waziri atuambie lini Serikali itaanza kutekeleza ujenzi wa barabara hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya kutoka J Corner – Mtiri – Sawala – Mgololo kutokufungwa kwa kiwango cha lami, ni vyema sasa Serikali ikafunga barabara hii kwa kiwango cha lami ambako kuna uchumi mkubwa wa viwanda kikiwemo kiwanda kikubwa kuliko vyote vya karatasi Afrika na Viwanda vya Chai zaidi ya vitano.

Mheshimiwa Naibu Spika, mawasiliano, nimeongea mara nyingi na Mheshimiwa Waziri kuhusu maeneo ambayo hayana mawasiliano ikiwamo maeneo ambayo minara imefungwa lakini haifanyi kazi kama mnara wa Mapanda, Kata ya Mapanda, mnara wa Vodacom haufanyi kazi na mnara wa Ikwiha, Kata ya Ikwiha haufanyi kazi, kwa hiyo, hakuna mawasiliano. Katika Vijiji vya Uhafiwa, Mapanda, Ukami, Ihimbo na Chogo pia Ikurha, Uginza, Ilangamoto, Ihamu, Isipii na Mpanga Tazara.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa uchukuzi, naomba sana Mheshimiwa Waziri waweke kituo cha abiria kwenye Kata ya Mpanga TAZARA, Kijiji cha Mpanga TAZARA, reli ya TAZARA.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.