Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Eng. Gerson Hosea Lwenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. ENG. GERSON H. LWENGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwa kuunga mkono hoja hii nzuri iliyowasilishwa na Mheshimiwa Waziri pia naipongeza sana Serikali ya Awamu ya Tano kwa kazi nzuri sana katika kuendeleza ujenzi, uchukuzi na mawasiliano. Naishukuru Serikali kwa kuanza ujenzi wa barabara ya kutoka Njombe - Moronga kilometa 53 iliyoko jimboni kwangu, nimeona zimetengwa shilingi bilioni 12 ambayo imeweza kujengwa takribani kilometa 12 tu kwa mwaka 2018/2019, ninatarajia utaliangalia ili kasi ya ujenzi iongezwe.

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Njombe - Ramadhani - Iyaji kilometa 74 imefanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina toka mwaka 2013 yapata miaka mitano sasa kazi ya ujenzi kwa kiwango cha lami haijauza. Nimefuatilia hotuba hii sijaona mahali wala fedha kutengwa ili kuanza kazi ya ujenzi kulingana na upembuzi huo uliofanyika. Je, ni lini kazi ya ujenzi itaanza? Je, wananchi waliowekewa alama za “X” za kijani ni lini watalipwa fidia ili kuruhusu kazi za ujenzi kuanza?

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Halali - Ilembule - Itulahumla nashukuru imetengewa fedha za matengenezo ya kawaida, lakini sijaona matengenezo ya Daraja la Halali ambalo limeathiriwa sana na mvua za mwaka huu. Naomba Serikali ifikirie kulijenga daraja jipya kwani ni jembamba sana na halijajengwa vizuri sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, Makao Makuu ya Wilaya yapo Igwichemya, mawasiliano ya simu yana kilometa mbili tu kwani ulienda zaidi ya kilometa tatu toka Igwachenya kwa mtandao ya Vodacom, Airtel, Tigo hakuna mawasiliano. Naomba Serikali irekebishe hali hii. Katika kuboresha viwanja vya ndege vya Milua, sijaona mpango wa kuboresha kiwanja cha ndege cha Njombe ili kiweze kuhudumia ndege kubwa. Katika bajeti ya mwaka 2017/2018 tuliahidiwa kuwa uwanja huu utaendelezwa. Naomba Mheshimiwa Waziri wakati unahitimisha hotuba hii niambie unasema nini kuihusu barabara ya Njombe (Ramadhani) Iyayi kujengwa kwa kiwango cha lami.