Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Prosper Joseph Mbena

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. PROSPER J. MBENA: Mheshimiwa Naibu Spika, napongeza jitihada kubwa zinazofanywa na Mheshimiwa Rais wetu mpendwa Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli katika kuliletea Taifa letu maendeleo ya kiuchmi. Miradi ya barabara ni muhimu sana katika kuleta maendeleo nchini. Kwa bahati mbaya sana katika hotuba ya Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano ya bajeti kwa mwaka wa fedha 2018/2019 barabara muhimu kwenye Jimbo la Morogoro Kusini hazikupewa fedha za kutekelezea miundombinu hiyo muhimu. Barabara ya kutoka Bigwa - Kisaki tulishakubaliana kwenye bajeti ya miaka miwili ya nyuma kwamba barabara hiyo itapanuliwa na kujengwa kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hiyo ilikuwa igharamiwe ujenzi wake kwa kiwango cha lami na Marekani kwenye mpango wa MCC II, lakini kutokana na sababu za kisiasa Marekani ilisitisha utekelezaji wake. Serikali yetu ikathibitisha kwamba itachukua jukumu la kugharamia mradi huo muhimu kwa faida ya wananchi na kuahidi Bungeni kwamba ndani ya miaka mitano, Serikali itajenga barabara hiyo ya Bigwa - Kisaki kwa kiwango cha lami. Inasikitisha kuona huu ni mwaka wa tatu wa miaka mitano Serikali bado haijaanza kutekeleza mradi huu. Kinachofanyika ni matengenezo tu, hili halikubaliki, fedha zilizotengwa kwenye bajeti ni matengenezo kwenye barabara ya udongo na changarawe, naiomba Serikali itekeleze ahadi yake.

Mheshimiwa Naibu Spika, ndani ya Jimbo la Morogoro Kusini, tunashida sana na barabara za udongo na changarawe zinazowatesa wananchi hususani wakati wa mvua. Barabara ya kwenda Kongwa, barabara ya Mvua – Magogoni – Selembala, barabara ya Mtombozi – Lugeni – Nemele, barabara ya Kangazi – Mtombozi, barabara ya Konde - Mlono (kilometa 4.5), barabara ya Matombo shuleni - Tawa, Matombo – Uponda.

Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo la Morogoro Kusini bado lina matatizo na mawasiliano ya simu. Haiwezekani katika karne hii, tunakuwa na wananchi kwenye vijiji vyetu vya Tanzania, haiwezekani kutumia simu zao kwa kukosa mtandao. Wengine inabidi wapande mitini ili kuzungumza na simu zao. Maeneo ya Kolero, Singisa, Bungu, Lugeni, Lusangalala, Uponda, Kasanga, Tandali na kadhalika wanahitaji huduma za simu hususani TTCL, Tigo, Airtel, Vodacom kilometa.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba Serikali itende haki kwa kugawa maendeleo kwa wananchi wetu sawa kwa sawa. Jimbo la Morogoro Kusini tunahitaji barabara za lami, fedha zinapotea nyingi kufanya matengenezo kwenye barabara za udongo kila mwaka, hiyo si sawa.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.