Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Hon. Ignas Aloyce Malocha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

MHE. IGNAS A. MALOCHA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa naipongeza Serikali kwa kazi kubwa inayoifanya katika Wizara hii. Tumeona mambo mengi na makubwa yanayofanyika, ujenzi wa reli, barabara, viwanja vya ndege, ununuzi wa ndege, meli na kadhalika. Hongereni sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, yapo maeneo mbalimbali au Mikoa ambayo haijabahatika kupitiwa na reli, iwe ya zamani au reli iliyojengwa kwa standard gauge. Mikoa hiyo ambayo haipitiwi na reli ipewe kipaumbele kuhakikisha inatengeneza barabara za Mikoa kwa kupitika vizuri ili wananchi waweze kusafirisha mazao yao kwa urahisi (mfano Mkoa wa Rukwa). Barabara ya Kibaoni – Kilyamatundu – Kamsamba itengenezwe kwa kiwango cha lami kwani barabara hii ina umuhimu mkubwa sana kiuchumi kwa wananchi na kwa Taifa zima kwa ujumla.

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Kalamba – Nzite – Ilemba ipanuliwe eneo la Mlimani kupunguza miinuko ya milima na kuweka zege eneo lote la Mlimani. Barabara ya Ntendo – Muze ijengwe kwa kwa kiwango cha lami. Eneo la Mlimani lipanuliwe, liwekewe kingo eneo la mlimani na mlima wote ujengwe kwa zege.

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Miangalua– Chombe nayo ipanuliwe eneo la Mlimani iwekewe zege eneo lote. Tunaomba ujenzi wa Daraja la Kilyamatundu – Kamsamba lijengwe haraka kama mkataba unavyojieleza.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naunga mkono hoja.