Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. COSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu viwanja vya michezo. Serikali ije na mkakati kabambe wa kupatikana viwanja vya Serikali vya michezo. Mfano katika Mkoa mpya wa Geita, Mkoa mzima hakuna viwanja vya football, basketball, netball na hata riadha. Pia nataka kufahamu mkakati wa Wizara kuhusu bima ya wanamichezo wote kwa kuwa hivi sasa mchezaji anapopata tatizo dogo la kiafya maisha yake yanakuwa ya kuombaomba. Kwa nini Wizara isipitie upya sera yake ili kuwafanya wanamichezo wote kuwa na hifadhi maalum ya fedha na bima kwa afya zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aina mbalimbali za michezo. Limekuwepo tatizo la Watanzania kuwekeza zaidi katika mpira wa miguu na kidogo ngumi ili kuongeza wigo au chaguo la aina ya michezo. Mfano shule ziache kuweka sharti la uwanja wa mpira wa miguu kama ishara ya kuwepo kwa michezo, ikiwezekana michezo kama kuogelea, ngumi, basketball, volleyball, table tennis na squash na mingine mingi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tushirikiane na Wizara ya Elimu kuratibu wamiliki wa shule kutoa proposal ya aina ya michezo ambayo shule itau-promote kwa nguvu zake zote kwa kuweka miundombinu yake badala ya kuweka mkazo kwenye masharti ambayo yamebaki kuwa mapambo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu vazi la Taifa, naishauri Serikali badala ya kulifanya vazi la Taifa kuwa moja kwa nchi nzima, vazi hili lianzie kwenye Wilaya, Mikoa na baadaye Taifa. Iwapo Wilaya kutakuwa na vazi lake na baadaye Mkoa mwisho wa siku Taifa litakuwa na vazi lenye kujumuisha Mikoa yote.