Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kodi zinazokusanywa kupitia sanaa nchini bado Serikali hii ya Awamu ya Tano imeshindwa kuwasaidia wasanii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, utaratibu wa kupata stika za TRA; ili kumwezesha msanii kuuza kazi yake kwa halali ni kwa nini Serikali inashindwa kuweka ofisi za usajili kila Wilaya na Mkoa ili kuondoa usumbufu kwa wasanii kwenda Dar es Salaam.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wizi wa kazi za wasanii na hati miliki. Mpaka sasa Serikali imeshindwa kuwasaidia wasanii, wanafanya kazi katika mazingira magumu mpaka akamilishe kazi yake sokoni, lakini kazi hiyo inaibiwa, inampelekea msanii kutopata faida na kufaidisha wezi wa kazi hizi. Je, ni lini Serikali itaona umuhimu wa wasanii pamoja na kulinda kazi zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa viwanja. Changamoto za viwanja vya michezo vingi vinamilikiwa na Chama cha Mapinduzi. Ni kwa nini Serikali inatumia kodi za wananchi hovyo kukarabati viwanja vya CCM ilihali viwanja hivi vingi nchini vina migogoro na kwa nini Serikali isichukue hatua ya kujenga viwanja vya michezo katika mikoa ili kuondoa ubaguzi huu na badala yake ijenge viwanja vya michezo katika mikoa na kuleta ajira, afya na michezo inawaweka watu pamoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Bunge Live; Serikali ya CCM imeshindwa kutetea hoja ya kwa nini Bunge halioneshwi na kupelekea wananchi kutoendelea kuiamini Serikali hii ya CCM kwa sababu inaficha mambo yake kupitia Bunge. Pia uminywaji wa demokrasia nchini kupitia vyombo vya habari kama radio, magazeti na kufungia nyimbo zinazokosoa Serikali, je, hawaoni kwa kufanya hivi ni kuonesha wamefeli.