Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Mussa Bakari Mbarouk

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Tanga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. MUSSA B. MBAROUK: Mheshimiwa Mwenyekiti, naanza kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia kuweza kuchangia katika Wizara hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mpira wa miguu na udhamini wa Serikali, Mpira wa miguu katika nchi yetu ya Tanzania ni mchezo unaopendwa lakini kwa bahati mbaya tumeshindwa kuwekeza katika michezo ipasavyo. Mfano katika Academy tupo nyuma sana, vilabu havina academies na shuleni hakuna mipango (mission wala vision) na hata ikiwepo dhaifu. Angalau tungeweza kuviandaa vilabu vyetu viwe na academies zao, hili nashauri vilabu vyote vilivyo katika VPL – Vodacom Premier League vielekezwe kuanzisha academies na Wizara ichangie. Vilabu vya Simba na Yanga kupewa mabasi na vilabu vingine kuachiwa huu utaratibu mbaya, vilabu vyote vinavyoshiriki VPL, vipatiwe usafiri (Buses).

Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee kuhusu wachezaji kukatwa kodi ya mapato. Wachezaji wa vilabu vyetu kukatwa kodi ni utaratibu mzuri lakini bado tuko mbali sana, kipato chao ni kidogo. Pawe na utaratibu wa kiwango fulani cha malipo na kwa muda maalum ukifika ndio wachezaji hawa wakatwe kodi. Mfano, mchezaji anayekuwa na mkataba unaoanzia Tsh. Milioni 100 kwa miaka mitatu mfululizo huyu akatwe kodi angalau asilimia tatu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, viwanja vya kisasa vya michezo, Jiji la Tanga lipo eneo la uwanja wa kisasa unaotaka kujengwa kwa ufadhili wa FIFA, hadi leo hakuna hata uzio na matokeo yake uwanja unaanza kuvamiwa na wajenzi holela. Je, Serikali katika ujenzi wa uwanja huu na udhamini wa FIFA inawaeleza Watanzania, mikataba ikoje, lini uwanja utaanza kujengwa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, michezo ya Kimataifa; mchezo wa boxing ndiyo mchezo pekee ambao unadiriki kututoa kifua mbele, lakini mchezo huu Wizara (Serikali) imeutupa, katika mikoa na wilaya ambazo mchezo huu unaendelea kuchezwa wapatiwe vifaa vya kisasa na vya kutosha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uibuaji vipaji shuleni, nashauri Serikali itilie maanani masuala ya michezo ya aina zote kuanzia primaries, secondary’s hadi Universities, Serikali ianze kuwekeza kwa dhati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, michezo ya Wabunge; pamekuwepo na mashindano ya Wabunge wa Afrika Mashariki, lakini maandalizi na stahiki za Wabunge wa Tanzania hazieleweki, wanadai kuanzia mashindano ya Mombasa (Kenya) hadi ilivyofanyika Dar es Salaam (Tanzania). Ushauri, namwomba Waziri atulipe Wabunge.