Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Susan Limbweni Kiwanga

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Mlimba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunachangia bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani pamoja na kuwa tutaipitisha lakini matumizi ya hizo pesa mpaka leo mimi sijajua. Kwa sababu hali ya utendaji kazi wa Jeshi la Polisi baadhi yao, sijui wanasema wanapata maagizo, kwa hiyo, hawafuati misingi yao, maelekezo na kanuni na maadili ya kazi zao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ni mmojawapo nimeathirika na utendaji wa Jeshi la Polisi, baadhi yao. Utakuta mkubwa kabisa eti anakuita, unasalimu amri unaenda kituo cha polisi, ukifika pale umesimama tena askari mwanaume anakupiga bonge la bao, yaani sijui wakoje mimi hata sielewi.

Hivi ukatili huu hawa watoto waliozaliwa na mwanamke kama mimi wanautoa wapi?

KUHUSU UTARATIBU . . .

MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, hilo neno la shetani nalitoa lakini hiyo message imeshafika. Kwa sababu kazi ya shetani ni kufanya mambo kinyume na binadamu na Mwenyezi Mungu anavyoamuru, nalitoa hilo neno la shetani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini uharamia huu unaofanywa na baadhi ya maaskari wanaochafua Jeshi la Polisi lazima tuuzungumze, hatuwezi kufumba macho. Kwa sababu tusipozungumza hata ukimwendea Mheshimiwa Mwigulu ukamwambia bwana kule kuna mambo haya anasema mambo mengine wanafanya kule mimi sijui. Huyu hapa anasema kwa sababu tunamwendea na tunampigia simu tunamwambia. Sasa leo nimepata nafasi kwa sababu imekuja bajeti lazima niseme. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hali ya mimi kama kiongozi, Mwenyekiti wa Chama, Mbunge wa Jimbo la Mlimba unataka kuongea na wananchi unawekewa barua pamoja na maelekezo sema hivi, sema hivi, ndiyo kazi ya Jeshi la Polisi? Siyo kazi ya Jeshi la Polisi, acha niseme, kama unaona nimekosa, kamata, weka ndani, nipeleke mahakamani, siyo kazi yako kunizuwia kusema mimi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hatuhitaji kupewa maelekezo kwa sababu sheria, kanuni na taratibu zipo. Tunahitaji kutoa taarifa siyo kuomba kibali, hivyo vibali, vibali ndiyo vinatupeleka huko tunakofika, watu wanajiona wana nguvu sana kuliko Katiba. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, je, ni kazi ya Jeshi la Polisi kwenda kuvamia kwenye lodge za watu ambao wanalipa kodi na kila kitu, usiku wa manane, eti kwa kisingizio hapa kulikuwa na watu mchana wamekaa wanataka kufanya maandamano ya tarehe 26, kimetokea Morogoro. Wanatoa wateja ndani wanawapiga, wanawaweka chini ya ulinzi, wanawalundika ndani, kuwaingiza hasara wafanyabiashara, huo ni uharamia, haukubaliki. Jeshi la Polisi fanyeni kazi zenu kwa weledi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hali ni mbaya, ukiuliza wanakwambia tumeagizwa.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)